Two
weeks ago, Tanzania’s second largest aid giver, withheld ten million dollars,
citing crackdown on homosexuality and alleged human rights abuses. According to
Reuters, Denmark, joined the World Bank whose decision not to release a $300
million loan, was made following
Tanzania’s recent “policy of banning pregnant girls from school and ...making
it a crime to question official statistics.” These developments are far
significant, yet today, we should discuss homosexuality.
Sunday, 17 March 2019
USING AID MONEY TO FORCE AFRICANS LEGALISE HOMOSEXUALITY...- Part Two
For Africans the outlook on
the subject is totally different from that of our counterparts in the rich
world. Homosexuality was and will always be a reality. A fact.
Yet, the problem (at the
moment) is not acceptance or not acceptance but, perception. The average
African views “being gay” in the “physical” sense. The actual words constantly
used on social media after Denmark’s announcement three weeks ago, were Sodom
and Gomorrah. To Whites (and all others who have legalised it) gay
lifestyle is viewed on a broader sense.
Not just as two people of the same gender agreeing to have sexual
intercourse, but as humans, loving each other. That is why prominent
individuals of the same gender openly
“marry” and live happily after. Check out famous musician Elton John and his
partner Mr David Furnish or Luxembourg Prime Minister, Xavier Bettel and Mr Gauthier
Destenay, tying knots, recently.
That is Europe.
Monday, 24 December 2018
SINEMA ZA NGONO ZINAVYO ATHIRI VIJANA ULIMWENGUNI LEO-3
Tuendelee na mada ya
Jumapili mbili zilizopita.
Tumezungumzia sinema za
ngono na namna zinavyohasidi afya na mahusiano ya watu. Sawa. Vipindi vya
maisha yetu wanadamu hutofautiana. Kama ambavyo makala hii inakashifu sinema za
ngono na changamoto zake ndivyo wazee wa miaka ile ya Sitini na Sabini
walivyokasirishwa na suruali za vijana zilizotanuka chini (“Pekos”) , na sketi
na magauni yaliyoishia mapajani (“Mini”).
Linganisha na leo. Vijana wanavalia suruali makalioni, kama wako
maliwatoni na wanawake wanaanika kabisa
kila kitu mitandaoni au maonesho.
SINEMA ZA NGONO ZINAVYO ATHIRI VIJANA ULIMWENGUNI LEO-2
Tuendelee na mada ya wiki
jana.
Zamani sinema za ngono
zilikatazwa kabisa na serikali ya Mwalimu Nyerere na hata awamu zilizofuata. Leo zinaonekana
waziwazi katika simu na wanawake kwa wanaume wanazikodolea macho. Matokeo kuna
kudhalilishana pande zote mbili. Hii ni kutokana na taswira za waigizaji
wachache wenye maungo yasiyofikana na hali halisi za wanadamu wengi.
Starehe hii kama zilivyo
nyingi za kisasa zimeletwa na utandawazi na teknolojia za Kizungu. Sisi
Waafrika hatukuwa na matatizo ya ngono au ufanyaji mapenzi. Mwalimu Nyerere na
viongozi waliopita wallifahamu hilo ndiyo maana wakalikataza.
Miaka 30 hadi 50 iliyopita
hatukuwa na matatizo ya mapenzi.
Nilipohamia Uzunguni nilishangazwa
jinsi wenzetu walivyo na matatizo makubwa ya ngono.
SINEMA ZA NGONO ZINAVYO ATHIRI VIJANA ULIMWENGUNI LEO - 1
Wakati Mwalimu Nyerere
akiwa Rais wetu, alisemwa vibaya, aliogopwa, alitaniwa. Ni ajabu namna leo, (nusu
karne baadaye) anazungumziwa kwa staha, tija na hata kupendekezwa aitwe
mtakatifu. Asiye na hatia au kosa. Sisi wanadamu wanafiki sana. Mtu akiwa nasi
tunamsuta. Akishatutoka tunamvalisha kila suruali, viatu, bangili na kofia za
jaha.
Nakumbuka tukiwa bado
sekondari, tulisafiri sana Nairobi kutembea. Miaka hiyo ya Sabini Kenya ilifananishwa
na Ulaya. Majuu. Nairobi ilijaa klabu
nzuri nzuri, mavazi ya Kizungu, sinema tele zikiwemo za ngono. Tuliwaona ndugu
zetu wa Kenya wenye bahati sana.
Tulimsikia Rais wao, Jomo
Kenyatta akisema: “Kuleni matunda ya Uhuru...”
Baadaye nilipokuwa mtu
mzima, nikasafiri Ulaya. Kwa mara ya kwanza nikaona sinema ya ngono, mwanzo hadi mwisho. Ilikuwa kioja. Sikuziona
nikiwa shuleni, ( tuliposafiri Kenya) shauri ya masharti ya kiumri. Ziliitwa
sinema za X. Yaani za watu wazima tu.
Sasa nikiwa Ughaibuni mtu
mzima niliyeshapitisha miaka 25 sikuzuiwa. Niliufurahia uhondo uliokatazwa na
Baba wa taifa na serikali ya TANU na CCM.
Lakini baada ya “kipya
kinyemi” kwisha, nikazoea, nikazikinahi.
Nilianza kugundua watu walioangalia filamu hizo walikuwa wanaume wapweke
wasiokuwa na wapenzi. Kila mtu alikaa peke yake, mle giza la sinema; akijishika
shika; wengine wakinywa pombe kisirisiri. Kifupi waliotazama michezo hii
walikuwa wapweke wenye matatizo ya kisaikolojia. Watu na wake zao
hawakuhudhuria sinema za ngono. Ndiyo walikuwepo wapenzi walioziangalia. Mmoja
mmoja na mkewe, lakini wachache...
Ziliitwa “pornography.”
Friday, 7 September 2018
... KUUHARIBU UHAI WETU KUPITIA MIMEA ILIYOBATILISHWA KWA GMO- Sehemu ya pili
Juma lililopita
tulifahamishana kuhusu GMO.
Kabla ya kuendelea
tukumbushane hulka ya biashara hususan huku nchi zilizoendelea. Siku hizi ni
kawaida kabisa kwa wateja, Uzunguni,
kutaka kujua nini wananunua, nini kitakachoingia tumboni, tarehe gani bidhaa itaoza au kukosa thamani, nk.
Wasiojali sana ni maskini au wasiosoma. Lakini hata hawa hulazimika kuchunguza pale maradhi yanapobisha hodi. Tutoe mfano...
Uzunguni kuna tatizo kubwa
la “allergies”
Allergies ni nini?
WIMBI LA MIMEA INAYOBATILISHWA KWA GMO
Miaka sitini (hadi 100) iliyopita-
sigara, ilivutia sana.
Sinema na TV ziliionyesha waigizaji wakiivuta mithili ya starehe ya hali ya juu sana.
Nikiwa kijana tuliambiwa mwanamke alipovuta sigara kisha akampulizia mwanaume
moshi usoni ni ishara ya kum-enzi, kumhitaji, kumtaka.
Sigara haikuonekana ni dhara.
Ila saratani
ilipounganishwa na sigara- makampuni ya tumbaku yalichachamaa. Mvutano huu wa
kibiashara ulichukua muda mrefu kupingika- hata mauaji na rushwa vilipita.
Vitisho. Ufisadi. Mabavu.
Subscribe to:
Posts (Atom)



