Monday 24 October 2011

US AND TOILETS –WHY DO WE DISLIKE EACH OTHER SO MUCH?

Just contemplating on the above subject is enough to give one jitters.
Without self analysis and critical examination, one cannot be honest. Honesty is a very expensive piece of information.

Like some proof?
Ask any wealthy person to give you the price for honesty…tell them you want truth at any cost. Watch their faces; listen to the tone of their voices. You will observe a certain degree of discomfort in their reaction.
Truth is annoying and that is why we had the hacking scandal via News of The World earlier this year. The owners of News of The World kept denying. Denial is the best weapon for avoiding the truth.
<--more--!>

Tuesday 4 October 2011

JE, KWANINI OMBI LA WAPALESTINA KUJIUNGA NA UMOJA WA MATAIFA NI MUHIMU KWETU SOTE?

Wiki iliyopita kiongozi wa Wapalestina, Mahmoud Abbas, alipigiwa makofi alipotoa hotuba ya dakika 35 kuutaka Umoja wa Mataifa uwatambue wananchi wake kama taifa huru.
“Wakati umefika, “ alieleza, “kwa wanaume, wanawake na watoto wetu kuwa na maisha ya kawaida. Kulala salama wakijua wataamka bila woga wa nini kitatokea kesho yake asubuhi.” 
Wapo waliompinga; mathalan Hamas, iliyodai kuna njia  bora zaidi kuwasukuma Wayahudi watambue haki za Wapalestina. Hamas ilisema Wapalestina lazima watumie nguvu kujikomboa badala “ya kuupigia magoti” Umoja wa Mataifa.

Mahmoud Abbas akiwa na bango la kiongozi maarufu wa Wapalestina Yasser Arafat....

Mrengo huo wa mawazo  unathibitishwa na Wamarekani walioshasema dhahiri kwamba watatumia kura ya “veto” ndani ya Baraza la Usalama kuzuia Wapalestina kuwa taifa huru. Kihistoria kura ya “veto” ilishatumika miaka ya nyuma kuyatia kabali masuala mbali mbali ya kimataifa. Iko mikononi mwa mataifa matano: Marekani, Uingereza, Urusi, Ufaransa na China.
<--more--!>