Thursday 16 June 2016

TUJIFUNZE NINI TOKA MAISHA NA HEKAYA ZA MUHAMMAD ALI ?



Bondia Muhammad Ali alipotembelea Tanzania mwaka 1980 akiwakilisha Marekani kuhusu michuano ya Olimpiki Moscow iliyokuwa na ukinzani. Kushoto kwake ni Thomas Mweuka wa Ofisi ya Habari Marekani Tanzania, USIS. Picha ya Mtandaoni.


Mwanadamu anapofariki huacha mali, watoto au maarifa. Mengi  yameandikwa ( na yataendelea kusemwa) kuhusu maisha ya bondia maarufu  Muhammad Ali aliyezikwa Alhamisi, Kentucky, Marekani.
  Wapo watu mashuhuri aina mbili.

Tuesday 7 June 2016

IT IS ALL ABOUT “BREXIT” UNTIL REFERENDUM DAY ON JUNE 23




Every season, new political words are created.
When President Barack Obama stepped into the ring of American power, in 2008, the phrase “Yes You Can” jumped up and accompanied his endearing smile. It does not matter whether the man has been successful or not...but this particular idiom is now part of the English vernacular.
Optimism.

SERA KUFUTA PLASTIKI TANZANIA SAMBAMBA NA HARAKATI ZA KIMATAIFA





 Mazingira machafu Tanzania- pic by Juma Gurumo, 2016

Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mheshimiwa January Makamba ametangaza kufutwa kabisa mifuko ya plastiki Tanzania mwakani. Agizo hili  linakwenda sambamba na kilio cha dunia nzima sasa hivi. Si tu Afrika ambapo mwamko wa kuyaweka mazingira katika hali ya usafi bado kushadidi vyema.

WIMBI KUBWA LA MATUMIZI YA NAZI NA MADAFU MAJUU







Zamani wakati nikikua tuliambiwa ukinywa  madafu utaota busha. Njoo sasa katika nazi na mapishi yake. Watoto wa kiume tulibezwa tulipokuna nazi. Nakumbuka enzi nikiishi kikapera Mwananyamala , Dar es Salaam nilitembelewa na dada fulani. Alipogonga mlango akanikuta nimekaa juu ya mbuzi nikikuna nazi hakustahimili.
“Freddy hebu uko...pisha nikusaidie.”
Ilikuwa miaka 40 iliyopita. Sina hakika kama leo mambo yamebadilika.