Monday 7 May 2012

UKEKETAJI WA WANAWAKE WAPIGIWA MADEBE UZUNGUNI

Majuma mawili yaliyopita gazeti mashuhuri  na aghali kuzidi yote  Uingereza- The Sunday Times lilitangaza habari moto zilizopeperushwa duniani kuhusu  akina mama zaidi ya laki moja Uingereza wanaodhalilishwa na ukeketaji. Gazeti hili lililoanzishwa mwaka 1821, lilifanya uchunguzi wa kisiri siri   kufichua waganga wa Kiafrika wanaotoza shilingi milioni mbili za hapa kumkeketa mwanamke mmoja. Kwa mujibu wa BBC wanawake husika  wanatoka  Yemen, Somalia, Eritrea na Ethiopia.
Ona mfano hapa...
  <--more--!>