Saturday 19 November 2022

SAIDI KANDA – VOICE OF TANZANIAN AND EAST AFRICAN ORIGINAL MUSIC

 


There is a reason we promote lions that climb trees in Lake Manyara. There is a reason countries have their own beloved songs. There are many reasons why tourists pay lots of money to go see Kangaroos in Australia or Moshi to scale Mount Kilimanjaro. And it is justified why we should pause and pay attention to a Tanzanian band called Mvula Mandondo Tolekaa. If you don't know what it means, please !Keep on reading. 


SUALA LA UVAAJI MIKANDA KATIKA MAGARI LASISITIZWA ULAYA


Mara ya kwanza kuvaa mkanda katika gari ilikuwa nilipopewa lifti  na Mzungu mmoja miaka ya Sabini. Kipindi hicho tuliwaita weupe, walami. Sijui neno lilitokea wapi. Ila yupo jamaa aliyefasiri kuwa “mlami” ilitokana na “lami” yaani barabara safi, isiyo ya matope, makorongo, udongo au mchanga. Barabara iliyowekwa lami ikawa ya Kizungu zungu. Na enzi hizo, walami waliangaliwa kama watu walioendelea. Si tu kitabia pia kiteknolojia. Ukiwa na mlami, unaulizwa maswali. Kakupa nini? Kakupeleka wapi, mlami? Atakupeleka mtoni? Yaani, utofauti.