Miaka sitini (hadi 100) iliyopita-
sigara, ilivutia sana.
Sinema na TV ziliionyesha waigizaji wakiivuta mithili ya starehe ya hali ya juu sana.
Nikiwa kijana tuliambiwa mwanamke alipovuta sigara kisha akampulizia mwanaume
moshi usoni ni ishara ya kum-enzi, kumhitaji, kumtaka.
Sigara haikuonekana ni dhara.
Ila saratani
ilipounganishwa na sigara- makampuni ya tumbaku yalichachamaa. Mvutano huu wa
kibiashara ulichukua muda mrefu kupingika- hata mauaji na rushwa vilipita.
Vitisho. Ufisadi. Mabavu.
