Showing posts with label Ubakaji na Sinema. Show all posts
Showing posts with label Ubakaji na Sinema. Show all posts

Monday, 24 December 2018

SINEMA ZA NGONO ZINAVYO ATHIRI VIJANA ULIMWENGUNI LEO-2


Tuendelee na mada ya wiki jana.
Zamani sinema za ngono zilikatazwa kabisa na serikali ya Mwalimu Nyerere  na hata awamu zilizofuata. Leo zinaonekana waziwazi katika simu na wanawake kwa wanaume wanazikodolea macho. Matokeo kuna kudhalilishana pande zote mbili. Hii ni kutokana na taswira za waigizaji wachache wenye maungo yasiyofikana na hali halisi za wanadamu wengi.
Starehe hii kama zilivyo nyingi za kisasa zimeletwa na utandawazi na teknolojia za Kizungu. Sisi Waafrika hatukuwa na matatizo ya ngono au ufanyaji mapenzi. Mwalimu Nyerere na viongozi waliopita wallifahamu hilo ndiyo maana wakalikataza.
Miaka 30 hadi 50 iliyopita hatukuwa na matatizo ya mapenzi.

Nilipohamia Uzunguni nilishangazwa jinsi wenzetu walivyo na matatizo makubwa ya ngono.