Tuendelee na mada ya
Jumapili mbili zilizopita.
Tumezungumzia sinema za
ngono na namna zinavyohasidi afya na mahusiano ya watu. Sawa. Vipindi vya
maisha yetu wanadamu hutofautiana. Kama ambavyo makala hii inakashifu sinema za
ngono na changamoto zake ndivyo wazee wa miaka ile ya Sitini na Sabini
walivyokasirishwa na suruali za vijana zilizotanuka chini (“Pekos”) , na sketi
na magauni yaliyoishia mapajani (“Mini”).
Linganisha na leo. Vijana wanavalia suruali makalioni, kama wako
maliwatoni na wanawake wanaanika kabisa
kila kitu mitandaoni au maonesho.
