Showing posts with label Ngono na Vijana. Show all posts
Showing posts with label Ngono na Vijana. Show all posts

Monday, 24 December 2018

SINEMA ZA NGONO ZINAVYO ATHIRI VIJANA ULIMWENGUNI LEO-3



Tuendelee na mada ya Jumapili mbili zilizopita.
Tumezungumzia sinema za ngono na namna zinavyohasidi afya na mahusiano ya watu. Sawa. Vipindi vya maisha yetu wanadamu hutofautiana. Kama ambavyo makala hii inakashifu sinema za ngono na changamoto zake ndivyo wazee wa miaka ile ya Sitini na Sabini walivyokasirishwa na suruali za vijana zilizotanuka chini (“Pekos”) , na sketi na magauni yaliyoishia mapajani (“Mini”).
 Linganisha na leo.  Vijana wanavalia suruali makalioni, kama wako maliwatoni  na wanawake wanaanika kabisa kila kitu mitandaoni au  maonesho.

SINEMA ZA NGONO ZINAVYO ATHIRI VIJANA ULIMWENGUNI LEO-2


Tuendelee na mada ya wiki jana.
Zamani sinema za ngono zilikatazwa kabisa na serikali ya Mwalimu Nyerere  na hata awamu zilizofuata. Leo zinaonekana waziwazi katika simu na wanawake kwa wanaume wanazikodolea macho. Matokeo kuna kudhalilishana pande zote mbili. Hii ni kutokana na taswira za waigizaji wachache wenye maungo yasiyofikana na hali halisi za wanadamu wengi.
Starehe hii kama zilivyo nyingi za kisasa zimeletwa na utandawazi na teknolojia za Kizungu. Sisi Waafrika hatukuwa na matatizo ya ngono au ufanyaji mapenzi. Mwalimu Nyerere na viongozi waliopita wallifahamu hilo ndiyo maana wakalikataza.
Miaka 30 hadi 50 iliyopita hatukuwa na matatizo ya mapenzi.

Nilipohamia Uzunguni nilishangazwa jinsi wenzetu walivyo na matatizo makubwa ya ngono.