Showing posts with label Prince Charles. Show all posts
Showing posts with label Prince Charles. Show all posts

Thursday, 2 April 2015

NASAHA KWA WATANZANIA WANAOULIZIA WAFADHILI NJE- Sehemu ya 3



Mti alionyongewa Mangi Meli Makindara wa Old Moshi mwaka 1892. Wakoloni wa Kijerumani waliua viongozi wengi. Mfano mzuri wa kumbukumbu toka Blog la Xanadu.

Toka niishi dunia ya  Wazungu nimejifunza jambo moja. Wenzetu wana mafanikio kwa sababu wanathamini sana vitu vyao. Hapa Uingereza hupenda kuhifadhi sana sanaa yao. Hata zile zilizoibiwa enzi za Ibilisi wa ukoloni, bado zimehifadhiwa.

NASAHA KWA WATANZANIA WANAOULIZIA WAFADHILI NJE- 2


Lipo tangazo linalorudiwa takriban kila kituo cha runinga huku Uzunguni, siku za karibuni. Tangazo humwonyesha mtoto mdogo wa kike, mweusi kama mpingo; mzuri ajabu, macho maangavu na uso uliotulia. Mwafrika. Watoto ni malaika, wahenga walisema. Na kweli wajihi wa msichana huyu wa Kimatumbi ni mkono wa Mungu. Namkisia ana miaka miwili au mitatu.