Showing posts with label Maendeleo Vijana. Show all posts
Showing posts with label Maendeleo Vijana. Show all posts

Monday, 17 June 2013

WATOTO WETU WANAVYOANZA KUATHIRIKA NA HALI YA KISIASA NCHINI


Wakati n’naishi Brazili miaka 20 iliyopita moja ya woga mkubwa ulioenea ni hatari ya watoto wadogo mijini. Hatari gani?
Sikiliza ...
Siku moja Jumapili  n’natembea ufukwe maarufu wa Copacabana  jijini Rio De Janeiro. Hapa pana eneo kubwa sana la kuogelea, wanawake warembo, majumba ya starehe, migahawa, magari, minazi na starehe za kuotea tu paukwa pakawa. Jaribu kulinganisha ufukwe huu na Coco Beach , Dar es Salaam. Anzia pale kilima kinachoelekea barabara ya Chake Chake ongoza hadi Kivukoni penye wauza samaki na boti linalovusha watu. Sema badala ya hospitali ya Ocean Road na Ikulu sasa weka majumba hayo niliyozungumzia ya starehe na sehemu ndefu  sana maridadi za kufanya mazoezi na kuogelea.
Watalii walipahusudu. Na hii si yote- ufukwe  wa Copacabana umeunganika na  Ipanema na Leblon, bichi nyingine mashuhuri za jiji. Wabrazili husema Mwenyezi Mungu aliuumba ulimwengu mzima kwa siku sita, ile ya saba akakaa kitako akikamilisha Rio De Janeiro peke yake. Nilikua na tabia ya kwenda kuogelea  na kufanya mazoezi pale mara mbili tatu kwa juma.

Wednesday, 11 May 2011

MTANDAO WA VIJANA TANZANIA : MAHOJIANO NA MICKEY “MIKIDADI” JONES MKAZI DENMARK NA LYDIA MKUDE ANAYESOMA, UGANDA...

Hali ngumu ya uchumi na maendeleo imezusha vijana wengi wasio na kazi; wanaranda randa ovyo barabarani, wakitega  na kusogoa vijiweni, wakijaribu hili na lile. Watoto yatima hawana wazazi kutokana na maafa ya maradhi ya Ukimwi na jamii yetu inazidi kukuuza wananchi wasiokuwa na matumaini. Yote haya yanaweza kumea hasira, kero na ghasia tupu.
Miezi michache Mickey Mikidadi Jones alikuwa likizo nyumbani. Hali ilimkuna sana.
Leo Mickey Mikidadi  Jones,  kaamua kujihusisha  na mtandao wa kuwaunganisha vijana  wa ughaibuni na kwetu Bongo kuboresha maisha yao. Mara nyingi nilipomhoji Mickey alimtupia maswali dada Lydia Mkude, ambaye ni mshauri mkuu wa MMVT ("Mtandao wa Maendeleo ya Vijana Tanzania").


Solomon Gaddi (mwenyekiti wa MMVT) akihutubia kikao. Kushoto kwake ni Haruna Mbeya (mwakilishi , Ughaibuni) na mwanzo kabisa Mshauri na mwakilishi wao wa kimataifa mtandaoni, Mickey Mikidadi Jones.   Picha ihsani ya MMVT.

 <--more--!>