Showing posts with label Mabasi Bongo. Show all posts
Showing posts with label Mabasi Bongo. Show all posts

Sunday, 14 May 2017

KILIO CHA WATOTO KARATU : TUENDELEE KUHUZUNIKA HADI LINI?


Ingawa muda umepita  tulioko Ughaibuni  tunawapa pole waliofiwa Karatu. Tumeangalia picha zilizosambazwa kwa uchungu, maastajabu na majonzi. Kama mzazi picha moja iliniuma sana. Watoto wa Lucky Vincent wamesimama  wakijitayarisha kuondoka safari yao ya mwisho.  Wamevalia mavazi ya shule: furaha ya mtoto. Masomo, maisha, matumaini. 
Ila picha inayostahili  kujadiliwa zaidi ni ya wanaume kadhaa wakikwea basi , wakijaribu kunyofoa maiti zilizojibana bana.  Hapa ndipo kilipo kilinge na janga letu Waafrika leo.

Wednesday, 9 November 2011

SANDUKU YATIMA NA SAFARI YANGU DODOMA KUELEKEA ARUSHA

Nilipokua nikiulizia basi la mikanda  Dodoma mjini;  jamaa mmoja akanicheka:
“We siku yako ya kufa ikifika utakufa tu…”
Na mimi pia  nikacheka nikikumbuka manabii walioandika maneno ya Mungu. Ndani ya sura ya saba ya Biblia mlango wa Mtakatifu Matayo tunashauriwa :
“Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombaye hupokea ; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.”
Niko Dodoma.
Nnasubiri kukata tiketi ya basi nielekee zangu mikoa ya kaskazi.
Uvaaji mikanda ndani ya magari bado unapuuzwa sana kwetu Afrika na nchi zinazoendelea...
 Baada ya kuzoea kuyapanda mabasi ya Kizungu niko kwetu Bongo nikizozana na itikeli, itikadi na desturi kidogo tofauti ambazo ingawa nilizaliwa na kukua nazo naziona kiasi fulani ngeni, za kutisha. Watanzania wenzangu wanakubali tu lile linalotokea na litokee. Mstari huo umezoeleka  kana kwamba Mtanzania anadhani maisha yake hayana faida tena; liwalo na liwe. Ni kama keshakata tamaa; ari ya mapigano inaanza kumnyauka; hana moyo.
<--more--!>