Showing posts with label Rosemary Mizizi. Show all posts
Showing posts with label Rosemary Mizizi. Show all posts

Sunday, 27 November 2011

MACHALARI MGOMBANI MOSHI NA NYAMA CHOMA ZA ARUSHA


Dunia yetu ina kila aina za udongo.
Udongo wa Mpirani nje kidogo ya Moshi mjini unanikumbusha wa Kigoma ambapo rangi yake inakurubia wekundu. Mimea ya Mpirani ni migomba, mapera, machungwa, ndimu, maembe, kahawa na gari analoendesha dada yangu Juliana linakwenda taratibu, likikwepa mashimo shimo ya udongo huu.


“Unaona ule msikiti?” naulizwa. Nikiwa mdogo haikuwepo misikiti mashambani Moshi.  Kidesturi migombani kwa Wachagga hujazana makanisa.
“Wapo mangi wengi Waislamu siku hizi,” dereva anafafanua.
<--more--!> 

Monday, 25 July 2011

BLOG LA “MWANAMKE NA NYUMBA” MFANO WA UANDISHI UNAOANGALIA MAHUSIANO NYETI YA MTANZANIA...

Uandishi wa mablogu wahitaji tarakilishi. Tarakilishi ni neno fasaha la Kiswahili linaloimanisha Kompyuta. Na hiki si chombo tu cha kuandikia. Huendesha simu za mkononi; taa zinazoongoza magari barabarani, mitambo ya ndege, mahospitali, runinga, nk. Dunia ya leo inaongozwa na tarakilishi. Hili ni bado somo jipya Tanzania. Kidunia mtandao kama tunavyoujua una miaka 15 ingawa sayansi hii ya kihabari imekuwepo kwa takribani miaka 30. Awali ilitumiwa na watu wachache hasa wanajeshi na majasusi kulinda matakwa ya serikali mbalimbali.
Rosemary Mizizi, blog lake Mwanamke na Nyumba linazungumzia mahusiano nyeti kati ya wanawake na wanaume  kwa undani sana katika jamii ya Tanzania leo.
<--more--!>