Ndiyo fikra inayonizonga nikiwa safarini Arusha kwenda Dar es Salaam. Mabasi yetu Bongo ni ramani nzuri ya kuujua utamaduni na jiografia ya miaka 50 baada ya Uhuru toka kwa Mwingereza. Ukiwa visiwani utasikia Taarabu na Kaswida; hapa Arusha hadi Moshi dereva katuwekea muziki wa Injili. Kama ile Kaswida inayoghani swalaa mbalimbali za Adhana (alfajiri) ya majogoo na Isha (mwisho jioni); nazisikia sifa kwa Yesu Kristo zikiliiza kwa jazba.
<--more--!>