Showing posts with label Imani na Usalama. Show all posts
Showing posts with label Imani na Usalama. Show all posts

Monday, 19 December 2011

INAHITAJIKA TENA KAMPENI YA “MTU NI AFYA” KUHIMIZA VYOO VISAFI AFRIKA

Kuna mambo ambayo kila jamii duniani huyahisi muhimu kuliko mengine. Kwa Mzungu akipita akaona mbwa yuko radhi achutame kumpapasa na kumpa  maneno mema. Kwetu kusalimiana wanadamu muhimu kuliko hidaya kwa wanyama.

Basi la "Baharia" mjini Moshi. Picha na F Macha

Ndiyo fikra inayonizonga nikiwa safarini Arusha kwenda Dar es Salaam. Mabasi yetu Bongo ni ramani nzuri ya kuujua utamaduni na jiografia ya miaka 50 baada ya Uhuru toka kwa Mwingereza. Ukiwa visiwani utasikia Taarabu na Kaswida; hapa Arusha hadi Moshi dereva katuwekea muziki wa Injili. Kama ile Kaswida inayoghani swalaa mbalimbali za Adhana (alfajiri) ya majogoo na Isha (mwisho jioni); nazisikia sifa kwa Yesu Kristo zikiliiza kwa jazba.
<--more--!>