Showing posts with label Wanawake Uingereza. Show all posts
Showing posts with label Wanawake Uingereza. Show all posts

Sunday, 20 December 2015

MGANGA MKUU UINGEREZA AONYA SIHA YA AKINA MAMA INAVYOTUATHIRI SOTE





Mganga mkuu Uingereza, Profesa Sally Davies, (pichani juu ) ,  amesisitiza umuhimu wa afya ya akina mama kwa taifa zima. Katika waraka aliouchapisha siku chache zilizopita-  kubadili kabisa mustakabal wa wanawake -Profesa Sally Davies alitaja mambo sita kisera na kiserikali. Mganga huyu aliye kati ya wanawake wachache wenye nguvu sana Uingereza ( kufuatana na kura ya Radio BBC 4, mwaka juzi), kitaaluma hushughulika na  maradhi ya damu, yaani “haematology”... 
Mfano mzuri wa jinsi damu inavyoathiri maumbile na afya yetu ni kama UKIMWI au saratani ya damu (“leukemia”) iliyomuua mwasisi wa taifa, Mwalimu Nyerere, 1999.