Showing posts with label Tiba. Show all posts
Showing posts with label Tiba. Show all posts

Thursday, 4 December 2014

WATANZANIA TUJIFUNZE KUWEKA AFYA MIKONONI, TUSISUBIRI KUDRA YA WAKUBWA AU MUNGU





 Miaka yote niliyosafiri na kuishi ughaibuni nimebaini siri moja  kuhusu afya. Wananchi wengi duniani hawaijali miili hadi wanapougua.  Zamani kidogo nilikuwa nikiongea na mganga wangu wa Kichina. Nilikwenda kuchomwa zile sindano zao zinazobandikwa sehemu mbalimbali mwilini na kuachwa zimesimama juu ya ngozi mithili ya mishale ya nungu nungu. Accupuncture (tamka “Akapan-kcha”), ndiyo jina lake la kitaalamu. Tiba hii iligunduliwa, kutafitiwa na kuendelezwa maelfu ya miaka kabla ya kuzaliwa Bwana Yesu Kristo na Mtume Muhammad SAW.   Kazi ya sindano hizi  ni kurekebisha na kusawazisha nguvu (au umeme) mwilini. Unapochomwa tatizo si maumivu. Haziumi kama sindano za Kizungu tulizozoea. Kinachochachafya ni vile Mchina anavyotafuta “njia sahihi.” Je, umewahi kushika waya wenye umeme? Unaukumbuka ule mstuko? Ukiwa mdogo, ndivyo  Accupuncture ilivyo. 
 Sindano za Kichina. Picha ya Mtandaoni
 

Wednesday, 27 April 2011

VIPI KISUKARI KINAWAUA WATANZANIA MAARUFU?

Habari kuhusu tiba ya Loliondo zimezigusa hisia za Watanzania wengi. Huku nje suala la mzee Mchungaji Ambilikile Mwasapile; halijafahamika vizuri. Wanahabari wachache tumefuatilia mambo ya “mti wa Loliondo” mitandaoni lakini si jambo la jazba kama nyumbani.  Suala lolote linalowasaidia wanadamu kuondokana na matatizo yao ya kimaisha huwa na umuhimu katika jamii. Loliondo imewika kutokana na afya zetu kuzidi kuwa mbaya. 
Waafrika tunatafuta majibu ya haraka.

Waingereza hutumia neno “Quick Fix” kuelezea ufafanuzi wa kupinda kona. Wabrazili husema “um jeitinho” (tamka, jeichinyo) kufumbua matatizo upesi upesi. Ni kama mtu huna hela ya chai ukala kiporo. Wachagga tuna chakula kinaitwa “Ikato”  (mseto wa maharage na ndizi);  badala ya mkate au maandazi.
<--more!-->