Showing posts with label Siasa na Sanaa. Show all posts
Showing posts with label Siasa na Sanaa. Show all posts

Sunday, 10 July 2011

SOMO KUTOKA MAISHA NA KIFO CHA MWANAMUZIKI GIL SCOTT-HERON

Je, pana faida gani kusikiliza habari za Mmarekani mweusi Gil Scott- Heron aliyefariki mwezi uliopita? Sidhani wapo Watanzania wengi seuze Waafrika waliomjua msanii huyu aliyetoa albam 15 za muziki na vitabu vitano; vitatu vya mashairi na riwaya mbili alizochapa akiwa bado shuleni. Gil Scott- Heron alipofariki Ijumaa Mei 27 akiwa na umri wa miaka 62, alibeba taji la mwasisi wa muziki wa Hip Hop na “Bob Dylan Mweusi.”
Gil Scott-Heron akitumbuiza na bendi yake "Amnesia Express" ukumbi wa Jazz Cafe, London mwaka 1999. Picha na F Macha
<--more--!>