Showing posts with label Saratani. Show all posts
Showing posts with label Saratani. Show all posts

Sunday, 30 November 2014

TEZI KIBOFU, AFYA NA KINGA YA MARADHI YANAYOTUKABILI -sehemu ya 1




Wiki hii,  Mheshimiwa Rais J Kikwete, alikuwa Marekani kufanyiwa matibabu ya tezi ya uume, hospitali ya John Hopkins,  Baltimore. Kitakwimu maradhi haya huwafika asilimia 45 ya wanaume walioshapitisha miaka 60.   Ingawa lengo la makala haya si kuzungumzia hali ya Rais, ni vizuri tukitathimini tatizo hili linalowasakama wanaume wengi. Miongoni mwa walioshafikwa ni marehem Nelson Mandela, kiongozi wa Waislamu Marekani, Louis Farahkan, mwanamuziki maarufu hayati James Brown, mwigizaji mashuhuri wa Hollywood, Robert De Niro, nk.
Miaka michache iliyopita niliwahi kuandika juu ya afya ya uume ( na uke vile vile) na kuhimiza haja ya kuelewa namna ya kutunza na kufanya mazoezi kutunza viungo hivi. Kwa wanaume viungo viwili muhimu husika ni mfuko wa mbegu (korodani) na tezi kibofu. Visipoangaliwa vyema husababisha saratani ambayo kihisabati,  inaua mwanaume mmoja kati ya  saba, duniani. Moja ya suluhisho kuu ni kuzifahamu dalili   kabla hazijaota kutu.  
Lakini tezi ya uume au tezi kibofu, ni nini hasa?