Wiki hii, Mheshimiwa Rais J Kikwete, alikuwa Marekani
kufanyiwa matibabu ya tezi ya uume, hospitali ya John Hopkins, Baltimore. Kitakwimu maradhi haya huwafika
asilimia 45 ya wanaume walioshapitisha miaka 60. Ingawa
lengo la makala haya si kuzungumzia hali ya Rais, ni vizuri tukitathimini
tatizo hili linalowasakama wanaume wengi. Miongoni mwa walioshafikwa ni marehem
Nelson Mandela, kiongozi wa Waislamu Marekani, Louis Farahkan, mwanamuziki
maarufu hayati James Brown, mwigizaji mashuhuri wa Hollywood, Robert De Niro, nk.
Miaka michache iliyopita
niliwahi kuandika juu ya afya ya uume ( na uke vile vile) na kuhimiza haja ya
kuelewa namna ya kutunza na kufanya mazoezi kutunza viungo hivi. Kwa wanaume
viungo viwili muhimu husika ni mfuko wa mbegu (korodani) na tezi kibofu. Visipoangaliwa
vyema husababisha saratani ambayo kihisabati, inaua mwanaume mmoja kati ya saba, duniani. Moja ya suluhisho kuu ni kuzifahamu
dalili kabla hazijaota kutu.
Lakini tezi ya uume au
tezi kibofu, ni nini hasa?
