“Mafanikio maishani yahitaji mawili; kutojua na kujiamini,” aliandika mtunzi maarufu wa riwaya, Mark Twain. Zamani shuleni tulisoma vitabu vya Mark Twain vinavyofundishia Kiingereza ulimwengu mzima. Kati ya riwaya ya sifa na sambusa ni The Adventures of Huckleberry Finn. Mashuhuri sana. Kisa chenye kejeli na utani kuhusu ubaguzi wa rangi. Nukuu, elimu na hekima za Mmarekani huyu aliyezaliwa mwaka 1835 akafariki 1910, (akatajirika kutokana na fasihi) hunyofolewa sana na wengi. Wanadamu tunapenda kujifunza kwa wenzetu waliofanikiwa kitaaluma na kimasilahi.
Mtunzi wa riwaya Mark Twain, mwaka 1871. Kitabu chake , Huckleberry Finn, hutumiwa mashuleni kujifunza Kiingereza ulimwengu mzima. Picha ya Wikipedia
Hebu tuikague nukuu hii kusaidia maongezi ya leo. Kutojua
kwaweza kuwa ujinga na Mwalimu Nyerere aliwahi kufafanua ifuatavyo...
