Wakati kampeni za uchaguzi zikiendelea miezi kadhaa iliyopita, Mtanzania mmoja mkazi London alikuwa na mtazamo tofauti. Mwanamuziki na mcheza sarakasi huyu anaitwa Fab Moses.
“Nyinyi semeni yenu mnayotaka, lakini CCM na Bw John
Pombe Magufuli watashinda tu.”
Fab Moses si maarufu kwa utabiri bali kwa ucha Mungu
wake, upole na ukarimu. Si wale wanaojifaragua au kupiga kelele mbele za watu.
Mtaratibu anayejishughulisha na kazi mbalimbali za ajira za uchovu tosha. Chukua mfano siku
niliyomtembelea kwake kumfanyia mahojiano haya. Ilibidi miadi ipangwe saa tisa
alasiri, maana aliingia kitandani asubuhi hiyo baada ya kazi ya usiku kucha.