Showing posts with label Julian Assange in Africa. Show all posts
Showing posts with label Julian Assange in Africa. Show all posts

Thursday, 20 September 2012

KINYAMKELA CHA MWANAHABARI JULIAN ASSANGE MJINI LONDON



 Niko katikati ya kitongoji cha matajiri, London...
Nimezungukwa na  majumba ya ghorofa, vigae, matofali ya kisasa,  vioo vitupu; mseto wa ujenzi. Punde nimekabiliana na Harrods-  duka maarufu la mamilionea  la ghorofa tano. Harrods imesimama mtaa wa Knightsbridge. Kando yake mna jumba dogo zaidi lenye  matofali rangi kikahawia mtindo wa karne ya kumi na tisa. Mtindo huu unalandana  na mila na desturi za Malkia Victoria aliyetawala karne hiyo (ya juzi) enzi za ukoloni. Nyanyake malkia Elisabeth.

Jengo lina ofisi nyingi na mojawapo ndipo ulipo Ubalozi wa Ecuador. Kawaida Ubalozi mdogo wa Ecuador usingekuwa na haja ya kuandikwa katika safu kama hii. Ila katika kipindi cha miezi miwili – umetajwa tajwa na kufahamika sana.
Hapa niliposimama nje nawaangalia askari zaidi ya kumi wa Kiingereza waliojipanga nje,wakiulinda ubalozi. Upande mwingine wamebana, paparazi na wanahabari na kamera zao; watalii wanapita pita nao wakipiga picha na mkabala wa Ubalozi limejikita kundi la watu, wakipiga kelele, wakiwasuta wale ma-askari. Mmoja wao kashika kipaaza sauti:
“Hakuna mtu aliyepiga simu namba 999 kuulizia msaada wenu, wajinga nyinyi!”
Askari hawasemi kitu. Watasema nini? Nchi hii ina Uhuru wa kusema na kujieleza.  Ukiyatazama mabango waliyobeba waandamaji  na mengine waliyoyabandika kando ya barabara pia mkabala na Ubalozi wa Ecuador, yatakufahamisha nini kinatokea. 
Mathalan:
“Kwanini askari wa Uingereza wanashirikiana na Marekani?”
“Ujasiri Unaambukiza!”
"Chapisheni Ukweli!"

“Uhuru.”
“Ondoeni mikono yenu toka Ecuador!”
“Serikali ya Uingereza ya Aibu lakini si wananchi wake!”
Na mabango kadhaa yana picha za mhusika.
“Mwacheni huru Assange! Msimpige Mjumbe risasi!”
 Yote, yumkini, yanamhusu mwanahabari Julian Assange ambaye toka Juni 19 aliomba ukimbizi  ubalozi wa Ecuador.

Friday, 31 August 2012

THE SAGA OF WIKILEAKS NEWSMAN JULIAN ASSANGE IN LONDON


Ambling  through the affluent areas of South West London I find myself at the famous Harrods shopping complex. Harrods towers above me like an old, crafty crocodile; where millionaires, the wealthy and royal buy stuff. It was created in 1834 and had many owners including Egyptian businessman Al Fayed whose son, Dodi, perished with Princess Diana in 1997. Two years ago this biggest (shopping) establishment in UK was sold to Qatar Prime Minister, Hamad bin Jassim bin Jaber Al Thani. (What a long name!) it is said the cost was one and half billion pounds.
Woow...

 Harrods soars over me as I marvel its amazing architecture. Wazungu always score with their buildings. They keep them fresh and forever. Many years ago while touring (with a theatre group) in Vienna, Austria I was mesmerised  how ancient pretty buildings still dazzle the city.
Like Zanzibar’s Stone Town, perhaps?
Author ambles around Stone Town in 2011...spooky and interesting
<--more--!>