Showing posts with label Adam Shafi. Show all posts
Showing posts with label Adam Shafi. Show all posts

Sunday, 30 October 2016

KISWAHILI KINAVYOZIDI KUPARAGANYA HERUFI “R” NA “ L”





Watanzania tuamke jamani. Tumelala.
....Kiswahili kilianzia kwetu. Nchi kumi na moja zinazungumza lugha hii iliyotuunganisha na kutuletea amani zaidi ya miaka 100!
 Nchi kumi na moja! Ongezea idhaa kadhaa za redio, TV na mitandao jamii ughaibuni inayokitukuza Kiswahili. Jazia, vyuo.
 Hapa London kiko chuo maarufu cha lugha- SOAS ( School of Oriental and African Studies- Shule ya Masomo ya Mashariki na Afrika).

Friday, 22 January 2016

KISWAHILI NOVELIST ADAM SHAFI SHEDS LIGHT ON AFRICAN AUTOBIOGRAPHIES





 I first met Zanzibar novelist, Adam Shafi in 1979.
He had just popped into then Tanzania Publishing House along Samora Avenue, downtown Dar es Salaam. His new book, Kuli, excited every Swahili reader and lover of literature. Kuli is a classic. Phenomenal. It is based on historical incidents during the colonial era in 1948. Port workers stage a strike that eventually contributes to Uhuru struggles for Zanzibar and Tanganyika (the older name of Tanzania) independence. 
Adam Shafi- pic by Mohammed Ghassani
 

Thursday, 13 February 2014

UBORESHAJI LUGHA NCHINI WATEGEMEA SANA WANAHABARI NA UJUZI WA FASIHI -1




Mzee Adam Shafi, mwandishi nguli aliyeanza shughuli zake kama mwanahabari zamani. Leo lazima kumsoma. Umahiri wake wa lugha hausemeki. Picha na F Macha, 2007.


Wiki iliyopita kulikuwa na mdahalo na majadiliano moto bungeni. Lugha ipi itumike kufundisha watoto wetu mashuleni? Tatizo hili si ngeni kwa nchi zinazotumia zaidi ya lugha moja kimawasiliano. Wakati ninaishi Canada miaka iliyopita niliepuka matatizo kwa vile kitongoji nilichoshukia kiliongea zaidi Kifaransa. Nilikuwa nimekwenda kusoma  mwaka mmoja. Kawaida Mtanzania unapofika  nchi isiyozungumza Kiingereza- hubidi utumie wastani wa mwaka mmoja kujifunza lugha. Haya yamewasibu wanafunzi waliokwenda Urusi, Ujerumani, China, Cuba nk.
Mwandishi nikifanya shughuli ya kutengeneza bustani, Canada, mwaka 1995...picha na S Vanessa.

Canada inazo lugha mbili : Kiingereza na Kifaransa.  Bahati  yangu wakati nikifanya kazi magazeti ya Uhuru na Mzalendo,  nilijifunza Kifaransa na ingawa ujuzi wa lugha hiyo si mzuri kama Kiingereza, ilinisadia sana masomoni.

Thursday, 4 April 2013

USONGO WANGU NA KISWANGLISHI : WATANZANIA HATUJAKOMAA KILUGHA-2


Kusoma na kutukuza fasihi  ya Kiswahili Fasaha kupitia vitabu na sinema  ndiyo njia pekee itakayoendeleza na kuimarisha lugha yetu...

Wiki jana tuliangalia namna ambavyo Kiswahili kimekua, kikazoa na kuburuta misamiati  ya lugha za Kiarabu, Kiingereza, Kiajemi, Kireno, Kihindi nk. Hapo hapo kanuni zake za kisarufi (“grammar”) ni za Kibantu. Ina maana Kiswahili ni lugha ya Kiafrika, inayojitosheleza.
Kukua kwa “Kiswanglish” si jambo baya. Tatizo hili si geni barani Afrika.Wala si geni ndani ya baadhi lugha mbalimbali ulimwenguni. Waspanyola wakazi wa Marekani wameunda “Spanglish”- lugha ya mitaani inayotumiwa  na walowezi waliozaliwa kule walio baina ya utamaduni wa Kimarekani na Kilatina. Tofauti ni kwamba Walatina huwalea wanao kufuata mila zao. Si kama Waafrika wengi wanaokulia Majuu- hawasisitizi wanao huku Uzunguni kuzijua mila na lugha zao. Wanaona nishai na aibu... kwamba lazima wafanane na wenyeji.
Amina Waziri ...mjukuu wa Shaaban Robert ambaye ni mmoja wa waalimu wakubwa wa Kiswahili Ughaibuni akiongea nami mwaka 2008 kuhusu haja ya kutukuza kumbukumbu ya babu yake na kuendeleza lugha hii muhimu. Picha na F Macha

Wiki jana tuliangalia namna Kenya ilivyoanza lugha ya Shenge, miaka 20 iliyopita. Lugha hii ilichanua kutokana na baadhi ya Wakenya-hasa mjini Nairobi- ambao ni wazungumzaji wazuri wa Kiingereza kuwa dhaifu katika msamiati wa Kiswahili na kuamua kuchanganya changanya. Lakini haina maana walikua duni lugha ya Kiingereza. Sisi tunaingiza Kiingereza katika Kiswahili- lakini tunasutwa (hasa na majirani wetu wa Kenya na Uganda) tulivyo wabovu kwa Kiingereza. Kabla ya kuendelea – hebu tuangalie nchi nyingine ya Kiafrika zenye mtindo wa kupikicha pikicha lugha kama Kenya.

Sunday, 30 January 2011

MTINDO WA KISASA WA NYWELE UNAHARIBU AFYA ZA WANAWAKE WEUSI

Watu wa kabila la Chwi kule Ghana wanaozungumza lugha iitwayo Tshi wana methali kuhusu umuhimu wa kupendeza. Inashauri: “Ikiwa mwenda wazimu ataiba nguo zako na kukimbia nazo wakati wewe uko majini unaoga, itakuwa vyema utafute angalau kipande cha kitambaa ujifunge wakati unamkimbiza maana usipofanya vile watazamaji watadhani na wewe umeheuka.”
Hakuna mwanaume ambaye hajawahi kupayukiwa kuwa asuburi wakati ndugu yake wa kike anajipodoa akijiremba. Na kati ya mapambo yote nywele zinaongoza foleni. Mwanaume waweza kutoka bila kuchana nywele, unaweza ukawa nusu kipara (kama mimi mwandishi) lakini hujali mradi u msafi utatoka zako mitaani. Kwa mwanamke kujisanifu nywele ni tendo muhimu sana. Ndiyo maana waandishi mbalimbali wa hadithi hawakosi maelezo ya ususi ndani ya riwaya zao.