Watu wa kabila la Chwi kule Ghana wanaozungumza lugha iitwayo Tshi wana methali kuhusu umuhimu wa kupendeza. Inashauri: “Ikiwa mwenda wazimu ataiba nguo zako na kukimbia nazo wakati wewe uko majini unaoga, itakuwa vyema utafute angalau kipande cha kitambaa ujifunge wakati unamkimbiza maana usipofanya vile watazamaji watadhani na wewe umeheuka.”
Hakuna mwanaume ambaye hajawahi kupayukiwa kuwa asuburi wakati ndugu yake wa kike anajipodoa akijiremba. Na kati ya mapambo yote nywele zinaongoza foleni. Mwanaume waweza kutoka bila kuchana nywele, unaweza ukawa nusu kipara (kama mimi mwandishi) lakini hujali mradi u msafi utatoka zako mitaani. Kwa mwanamke kujisanifu nywele ni tendo muhimu sana. Ndiyo maana waandishi mbalimbali wa hadithi hawakosi maelezo ya ususi ndani ya riwaya zao.
Showing posts with label Waafrika. Show all posts
Showing posts with label Waafrika. Show all posts
Sunday, 30 January 2011
Monday, 27 December 2010
SUALA LA MAZOEZI YA UINUAJI VYUMA KWA WABONGO
Baada ya kuandika kuhusu maradhi ya moyo na kichomi yanavyodhalilisha vijana leo, mwezi Novemba, Watanzania wengi waliniandikia kutaka ufafanuzi kuhusu mazoezi na uinuaji vyuma. Mazoezi na uinuaji vyuma ni mada muhimu sana.
Suala la kwanza ambalo pia limeenea barani Afrika ni kwamba kazi ngumu (sulubu) ni sawa na mazoezi. Eti kama mtu anatembea kwenda kazini au anayo maisha ya taabu yanayoutoa mwili jasho kila siku basi hilo ni zoezi tosha.
Suala la kwanza ambalo pia limeenea barani Afrika ni kwamba kazi ngumu (sulubu) ni sawa na mazoezi. Eti kama mtu anatembea kwenda kazini au anayo maisha ya taabu yanayoutoa mwili jasho kila siku basi hilo ni zoezi tosha.
Subscribe to:
Posts (Atom)