Showing posts with label Mwananchi. Show all posts
Showing posts with label Mwananchi. Show all posts

Wednesday, 30 March 2011

KITABU KINACHOELEZEA YALIYOWAFIKA WAPINZANI TANZANIA CHATOKA UINGEREZA...

Kina kurasa 272.
Toka nchi yetu iwe huru miaka hamsini sasa hajatokea Mtanzania akaandika kitabu cha aina hii.  Watanzania tunaogopa. Hofu hiyo imeenea miaka mingi na imetushika hata sisi wanahabari wenyewe.
<--more!-->

Sunday, 9 January 2011

KUJIENDELEZA, MAZOEZI NA KUINUA VYUMA -Sehemu ya Mwisho

Makala kadhaa zilizopita zimesisitiza sisi wananchi wenyewe kujiendeleza. Lengo la insha hizi ni kukumbusha wewe mwananchi kwamba huwezi kusonga mbele bila elimu na maarifa sahihi; kwamba maendeleo yanawezekana.
Jamii ya Marekani imejenga utamaduni huu uitwao Self Help. Ni utamaduni uliozalisha biashara ya vitabu, video, magazeti na vipindi mbalimbali vya runinga vinavyosisitiza mwananchi kujituma badala ya kutegemea uchawi, dini au imani nyingine peke yake. Lengo ni kuweka nguvu za kimaendeleo mikononi mwa mwanadamu. Kelele inayopigwa ndani ya utamaduni wa Kimarekani ni kuwa lolote linawezekana kwa anayejitahidi.

Monday, 27 December 2010

SUALA LA MAZOEZI YA UINUAJI VYUMA KWA WABONGO

Baada ya kuandika kuhusu maradhi ya moyo na kichomi yanavyodhalilisha vijana leo, mwezi Novemba, Watanzania wengi waliniandikia kutaka ufafanuzi kuhusu mazoezi na uinuaji vyuma. Mazoezi na uinuaji vyuma ni mada muhimu sana.
Suala la kwanza ambalo pia limeenea barani Afrika ni kwamba kazi ngumu (sulubu) ni sawa na mazoezi. Eti kama mtu anatembea kwenda kazini au anayo maisha ya taabu yanayoutoa mwili jasho kila siku basi hilo ni zoezi tosha.

Sunday, 26 December 2010

MUSICIAN REMMY ONGALA - Obituaries in English and Swahili

FOUR PHASES IN THE LIFE OF REMMY ONGALA AND RECALLING HIS LAST GIG IN LONDON

I would like to divide the life of excellent musician Remmy Ongala who died on Sunday night into four phases. First, his early years growing and entertaining in Kivu, Eastern Zaire where he was born on February 10th, 1947. Those grounding years included playing guitar, kit drums and saxophone. This passion for music was pushed by sadness. Both parents died when he was quite young; his father, Etiennes Kalimangonga was a percussion player while his charismatic mother, Aziza Moza Mayokei passed away in 1964 leaving the lonely boy heart broken in standard five.
The late genius musician, Rama  Zani Mtoro Ongala, was a man of incredible lyrical skill...