Showing posts with label Masudi Pashamoto Msele. Show all posts
Showing posts with label Masudi Pashamoto Msele. Show all posts

Sunday, 30 October 2016

KISWAHILI KINAVYOZIDI KUPARAGANYA HERUFI “R” NA “ L”





Watanzania tuamke jamani. Tumelala.
....Kiswahili kilianzia kwetu. Nchi kumi na moja zinazungumza lugha hii iliyotuunganisha na kutuletea amani zaidi ya miaka 100!
 Nchi kumi na moja! Ongezea idhaa kadhaa za redio, TV na mitandao jamii ughaibuni inayokitukuza Kiswahili. Jazia, vyuo.
 Hapa London kiko chuo maarufu cha lugha- SOAS ( School of Oriental and African Studies- Shule ya Masomo ya Mashariki na Afrika).