Showing posts with label Kenya na Kiswahili. Show all posts
Showing posts with label Kenya na Kiswahili. Show all posts

Saturday, 12 November 2016

KISWAHILI KINAVYOPARAGANYA HERUFI “R” NA “ L”- 2



Tatizo la Kiswahili kuanza kudidimia siku hizi linatokana na sababu nyingi. Juu kabisa ni Watanzania  kutojielewa kinafsiya. Ndiyo tunajijua sisi Watanzania. Tunaishi wapi kijiografia. Lakini sidhani tunaelewa vizuri nafasi yetu kitamaduni hapa duniani. Matumizi yetu ya lugha yanaonesha “kuchanganyikiwa” huku kunakodhihirisha ulimbukeni fulani.
Miye Mtanzania siogopi kujitoboa jicho.
Chukua mfano wa mitandao jamii. Mtanzania atatoa maoni fulani tuseme ukuta wa Facebook.  Labda jambo zuri limeandikwa kwa  Kiswahili. Kujionesha ataandika maoni yake  Kiingereza au Kiswanglish. Au jambo limeandikwa Kiingereza, yeye ataweka maoni Kiswahili.


Sunday, 30 October 2016

KISWAHILI KINAVYOZIDI KUPARAGANYA HERUFI “R” NA “ L”





Watanzania tuamke jamani. Tumelala.
....Kiswahili kilianzia kwetu. Nchi kumi na moja zinazungumza lugha hii iliyotuunganisha na kutuletea amani zaidi ya miaka 100!
 Nchi kumi na moja! Ongezea idhaa kadhaa za redio, TV na mitandao jamii ughaibuni inayokitukuza Kiswahili. Jazia, vyuo.
 Hapa London kiko chuo maarufu cha lugha- SOAS ( School of Oriental and African Studies- Shule ya Masomo ya Mashariki na Afrika).