Tatizo la Kiswahili kuanza kudidimia siku hizi linatokana
na sababu nyingi. Juu kabisa ni Watanzania
kutojielewa kinafsiya. Ndiyo tunajijua sisi Watanzania. Tunaishi wapi
kijiografia. Lakini sidhani tunaelewa vizuri nafasi yetu kitamaduni hapa
duniani. Matumizi yetu ya lugha yanaonesha “kuchanganyikiwa” huku kunakodhihirisha
ulimbukeni fulani.
Miye Mtanzania siogopi kujitoboa jicho.

