Showing posts with label Lugha na Maendeleo. Show all posts
Showing posts with label Lugha na Maendeleo. Show all posts

Saturday, 12 November 2016

KISWAHILI KINAVYOPARAGANYA HERUFI “R” NA “ L”- 2



Tatizo la Kiswahili kuanza kudidimia siku hizi linatokana na sababu nyingi. Juu kabisa ni Watanzania  kutojielewa kinafsiya. Ndiyo tunajijua sisi Watanzania. Tunaishi wapi kijiografia. Lakini sidhani tunaelewa vizuri nafasi yetu kitamaduni hapa duniani. Matumizi yetu ya lugha yanaonesha “kuchanganyikiwa” huku kunakodhihirisha ulimbukeni fulani.
Miye Mtanzania siogopi kujitoboa jicho.
Chukua mfano wa mitandao jamii. Mtanzania atatoa maoni fulani tuseme ukuta wa Facebook.  Labda jambo zuri limeandikwa kwa  Kiswahili. Kujionesha ataandika maoni yake  Kiingereza au Kiswanglish. Au jambo limeandikwa Kiingereza, yeye ataweka maoni Kiswahili.