Showing posts with label Fasihi na Lugha. Show all posts
Showing posts with label Fasihi na Lugha. Show all posts

Thursday, 13 February 2014

UBORESHAJI LUGHA NCHINI WATEGEMEA SANA WANAHABARI NA UJUZI WA FASIHI -1




Mzee Adam Shafi, mwandishi nguli aliyeanza shughuli zake kama mwanahabari zamani. Leo lazima kumsoma. Umahiri wake wa lugha hausemeki. Picha na F Macha, 2007.


Wiki iliyopita kulikuwa na mdahalo na majadiliano moto bungeni. Lugha ipi itumike kufundisha watoto wetu mashuleni? Tatizo hili si ngeni kwa nchi zinazotumia zaidi ya lugha moja kimawasiliano. Wakati ninaishi Canada miaka iliyopita niliepuka matatizo kwa vile kitongoji nilichoshukia kiliongea zaidi Kifaransa. Nilikuwa nimekwenda kusoma  mwaka mmoja. Kawaida Mtanzania unapofika  nchi isiyozungumza Kiingereza- hubidi utumie wastani wa mwaka mmoja kujifunza lugha. Haya yamewasibu wanafunzi waliokwenda Urusi, Ujerumani, China, Cuba nk.
Mwandishi nikifanya shughuli ya kutengeneza bustani, Canada, mwaka 1995...picha na S Vanessa.

Canada inazo lugha mbili : Kiingereza na Kifaransa.  Bahati  yangu wakati nikifanya kazi magazeti ya Uhuru na Mzalendo,  nilijifunza Kifaransa na ingawa ujuzi wa lugha hiyo si mzuri kama Kiingereza, ilinisadia sana masomoni.

Saturday, 30 November 2013

MASHUJAA WAWILI WA MFANO WALIOFARIKI MWEZI NOVEMBA…


Tarehe 23 Novemba 1963 wakati namalizia malizia darasa la pili,  tuliambiwa tusiende shule. Jana yake, Rais John F Kennedy wa Marekani alipigwa risasi akiwa ziarani mjini Texas. Nakumbuka Watanganyika (tulivyoitwa miaka hiyo ) tulivyosikitika. Rais Kennedy alipendwa sana. Marekani iliisaidia Tanganyika kwa  misaada na wataalamu wa kujitolea – walioitwa “Peace Corps.” Urafiki huu ulidhihirishwa na mifuko ya sembe na vyakula yenye picha ya mkono wa Mzungu na Mwafrika vimeshikana kirafiki.
Mwalimu Nyerere alipokaribishwa  na Rais John Kennedy na kuhutubia Ikulu ya Marekani- mwaka 1963. Walikuwa marafiki wakubwa. Miezi michache baadaye Rais Kennedy aliuawa.

Baada ya miaka mitano mdogo wake marehem, Robert F Kennedy naye aliuliwa kwa risasi wakati akifanya kampeni za Urais. Wengi walitazamia angekuwa kiongozi bora kama kaka mtu.
Toka walipouawa ndugu hawa, sinema mbalimbali na mandishi yametolewa kuhusu kisa na sababu. Aliyezungumziwa na anayeendelea kuongelewa ni marehem John Kennedy- rais aliyependwa kuzidi wote katika historia ya Marekani.