Showing posts with label Wahadhiri na Waalimu. Show all posts
Showing posts with label Wahadhiri na Waalimu. Show all posts

Sunday, 17 March 2019

KISWAHILI CHETU KINADIDIMIZWA NA KUPANDISHWA NA NANI?


Nilimhoji Mkenya mmoja kwa kipindi  cha Kwa Simu Toka London. Jina nitalihifadhi kwa sasa. 
“Nikiwa mdogo sikupenda kabisa kwetu Kenya tulivyolazimishwa kujifunza Kiingereza.  Tulichapwa...”
Nikasema ndiyo maana Kenya na  Waafrika wengine huzungumza Kiingereza  ( na lugha zingine za Kizungu ) kwa ufasaha sana.
“Lakini nilipofika hapa Uingereza nilishangaa au tuseme nikajifunza. Waingereza wanaipenda sana lugha yao.  Huongea tofauti na sisi tunavyoongea. Ukitaka uraia wa Uingereza lazima ujue Kiingereza sawasawa.  Wanakithamini Kiingereza. Majina, barabara, shule, serikali, muziki,magazeti, vitabu, kila kitu.  Hawatumii lugha nyingine. Hawakidunishi. Wala hawakichanganyi na lugha nyingine. Nikatafakari. Ndipo nikaanza kuifikiria Tanzania...”
Akadai miaka mingi amependa sana msimamo wa Watanzania.
  “Zipo nchi kumi na moja zinazungumza Kiswahili. Lakini chimbuko la Kiswahili ni Tanzania. Hata wengine tukijidai, hatuifikii Tanzania...”
Mara, mhojiwa akapaaza sauti.

Thursday, 13 February 2014

WAALIMU NA WAHADHIRI WANALO JUKUMU KUBWA KUENDELEZA ELIMU AFRIKA


Kufuatana na kampuni maarufu ya huduma za uhasibu, Ernst na Young, yenye makao makuu London, kuanzia mwaka 2,000 hadi 2015,  Afrika iko katika maendeleo makubwa  kiuchumi. Ingawa sisi wenyewe tunajihisi hali mbaya, ulimwengu mzima unalitegemea bara  kwa mali asili na hali ya hewa.
Na hayakuanza leo. Baada ya mkutano maarufu wa Berlin ,  1884- chini ya uenyekiti wa Mfalme Otto Von Bismarck- wakoloni walikuja, wakaondoka.  Watawala wenyeji wakaendeleza uzi ule ule wa kikoloni: kupora; wakishirikiana na wakubwa; wakihadaa kwa maneno maneno na bunduki. Dunia nzima inatushangaa vipi, sisi matajiri wa mali ghafi, bado tunategemea misaada; vita vya wenyewe kwa wenyewe, magaidi wanaua hadi wanafunzi na watoto : Nigeria. Wanawake wanabakwa, Kongo, Sudan na Jamhuri ya Afrika ya Kati.  Kwa maskini asiye na mali au nguvu za kisiasa, elimu tu ndiyo ubwabwa uliosalia.  
Asili mia ndogo sana wanafikia shahada ya mwanzo  (Bachelors) au  Diploma; na  kidogo zaidi kuendelea shahada ya kati (Masters), uzamili.
Kama Francis Magomeni(jina la bandia) aliyekuja kusoma shahada ya uzamili (uchumi), London, karibuni.
“Nataka niwe kama akina Profesa Lipumba, Profesa Palagamba Kabudi,  Profesa Muhongo. Si lazima niwe Waziri, lakini niwe fresh.  Nchi yetu yahitaji wataalamu.  Wakenya, Uganda, Burundi wanachukua kazi zote, kwa vile sisi hatujasoma.”

Hayati Nyerere. Mwanaelimu na mwalimu maarufu kuzidi wote katika historia ya Tanzania.
Picha ya Wikipedia....