Nilimhoji
Mkenya mmoja kwa kipindi cha Kwa Simu
Toka London. Jina nitalihifadhi kwa sasa.
“Nikiwa
mdogo sikupenda kabisa kwetu Kenya tulivyolazimishwa kujifunza Kiingereza. Tulichapwa...”
Nikasema
ndiyo maana Kenya na Waafrika wengine huzungumza
Kiingereza ( na lugha zingine za Kizungu
) kwa ufasaha sana.
“Lakini
nilipofika hapa Uingereza nilishangaa au tuseme nikajifunza. Waingereza
wanaipenda sana lugha yao. Huongea tofauti
na sisi tunavyoongea. Ukitaka uraia wa Uingereza lazima ujue Kiingereza
sawasawa. Wanakithamini Kiingereza.
Majina, barabara, shule, serikali, muziki,magazeti, vitabu, kila kitu. Hawatumii lugha nyingine. Hawakidunishi. Wala
hawakichanganyi na lugha nyingine. Nikatafakari. Ndipo nikaanza kuifikiria
Tanzania...”
Akadai
miaka mingi amependa sana msimamo wa Watanzania.
“Zipo nchi kumi na moja zinazungumza
Kiswahili. Lakini chimbuko la Kiswahili ni Tanzania. Hata wengine tukijidai,
hatuifikii Tanzania...”
Mara,
mhojiwa akapaaza sauti.