Showing posts with label Wahadhiri Kiswahili. Show all posts
Showing posts with label Wahadhiri Kiswahili. Show all posts

Sunday, 17 March 2019

KISWAHILI CHETU KINADIDIMIZWA NA KUPANDISHWA NA NANI?


Nilimhoji Mkenya mmoja kwa kipindi  cha Kwa Simu Toka London. Jina nitalihifadhi kwa sasa. 
“Nikiwa mdogo sikupenda kabisa kwetu Kenya tulivyolazimishwa kujifunza Kiingereza.  Tulichapwa...”
Nikasema ndiyo maana Kenya na  Waafrika wengine huzungumza Kiingereza  ( na lugha zingine za Kizungu ) kwa ufasaha sana.
“Lakini nilipofika hapa Uingereza nilishangaa au tuseme nikajifunza. Waingereza wanaipenda sana lugha yao.  Huongea tofauti na sisi tunavyoongea. Ukitaka uraia wa Uingereza lazima ujue Kiingereza sawasawa.  Wanakithamini Kiingereza. Majina, barabara, shule, serikali, muziki,magazeti, vitabu, kila kitu.  Hawatumii lugha nyingine. Hawakidunishi. Wala hawakichanganyi na lugha nyingine. Nikatafakari. Ndipo nikaanza kuifikiria Tanzania...”
Akadai miaka mingi amependa sana msimamo wa Watanzania.
  “Zipo nchi kumi na moja zinazungumza Kiswahili. Lakini chimbuko la Kiswahili ni Tanzania. Hata wengine tukijidai, hatuifikii Tanzania...”
Mara, mhojiwa akapaaza sauti.