Kufuatana na kampuni maarufu ya
huduma za uhasibu, Ernst na Young, yenye makao makuu London, kuanzia mwaka
2,000 hadi 2015, Afrika iko katika
maendeleo makubwa kiuchumi. Ingawa sisi wenyewe
tunajihisi hali mbaya, ulimwengu mzima unalitegemea bara kwa mali asili na hali ya hewa.
Na hayakuanza leo. Baada ya mkutano
maarufu wa Berlin , 1884- chini ya uenyekiti
wa Mfalme Otto Von Bismarck- wakoloni walikuja, wakaondoka. Watawala wenyeji wakaendeleza uzi ule ule wa
kikoloni: kupora; wakishirikiana na wakubwa; wakihadaa kwa maneno maneno na
bunduki. Dunia nzima inatushangaa vipi, sisi matajiri wa mali ghafi, bado
tunategemea misaada; vita vya wenyewe kwa wenyewe, magaidi wanaua hadi
wanafunzi na watoto : Nigeria. Wanawake wanabakwa, Kongo, Sudan na Jamhuri ya
Afrika ya Kati. Kwa maskini asiye na
mali au nguvu za kisiasa, elimu tu ndiyo ubwabwa uliosalia.
Asili mia ndogo sana wanafikia
shahada ya mwanzo (Bachelors) au Diploma; na kidogo zaidi kuendelea shahada ya kati
(Masters), uzamili.
Kama Francis Magomeni(jina la
bandia) aliyekuja kusoma shahada ya uzamili (uchumi), London, karibuni.
“Nataka niwe kama akina
Profesa Lipumba, Profesa Palagamba Kabudi, Profesa Muhongo. Si lazima niwe Waziri, lakini
niwe fresh. Nchi yetu yahitaji wataalamu. Wakenya, Uganda, Burundi wanachukua kazi
zote, kwa vile sisi hatujasoma.”
Hayati Nyerere. Mwanaelimu na mwalimu maarufu kuzidi wote katika historia ya Tanzania.
Picha ya Wikipedia....