Showing posts with label Mapenzi na Wageni. Show all posts
Showing posts with label Mapenzi na Wageni. Show all posts

Monday, 18 August 2014

KWA WANAOLILIA MAPENZI NA WAGENI AU WAZUNGU- Sehemu ya 2...


 Karibuni rafiki yangu Mzungu alikuwa Afrika.
Taaluma yake ni uanahabari.  Anaipenda sana Afrika na watu wake. Zamani babu aliishi India na alipinga sana ukoloni. Ana mke  na watoto wawili. Shughuli zake humzungusha kila sehemu.  Analijua bara kuliko hata tuliozaliwa huko.  Baada ya  sifa na vicheko, ghafla alisuta mapenzi.
“Ningekuwa mmoja wa babu zenu zamani Bwana Freddy ningenyaka wake ishirini. Kila  nilikokwenda sikukosa sahiba.  Wanataka niwatumie tikiti za ndege. Waje Ulaya waishi raha mustarehe. Ni vigumu sana kuwahimiza dada hawa kwamba maisha yangu si ya kitajiri. Hata ningekuwa tajiri kwetu Ulaya ndoa za mitala haziruhusiwi.  Na mke wangu hatofurahi akisikia nina wake wengine!”
Inachekesha alivyosema, lakini ndiyo kichuguu cha mchwa hicho.

KWA WANAOLILIA MAPENZI NA WAGENI AU WAZUNGU...- Sehemu ya 1

Miaka ya karibuni  wananchi wengi- hususan vijana- wameulizia mahusiano ya kimapenzi na wageni  hasa Wazungu. Hayakuanza leo, jana wala juzi. Yamekuwapo daima. Ukweli idadi fulani ya watu wa mataifa yote duniani hutaka kuwa na mahusiano na wageni. Mosi, kutaka kuondokana na udhia wa wananchi wenzao; pili, kutafuta maisha bora; tatu,mapenzi na ndoa na nne, udadisi (kipya kinyemi).
Mwandishi nikitumbuiza ngoma wakati wa  Carnival  la London, Agosti, 2012.

Miaka arobaini au hamsini iliyopita nakumbuka waliopenda mahusiano na wageni walikuwa zaidi wanaume. Wanawake waliojamiiana na wageni waliitwa malaya, na wachache ni wale tu waliofanya kazi mahoteli makubwa ya kitalii kutafuta ajira. Mathalan nakumbuka miaka ya Sitini na Sabini, Tanzania ilijazana wakimbizi. Sera ya TANU na siasa ya Azimio la Arusha ilisaidia walioathirika na udhalimu wa kikoloni, ubaguzi nk. Toka Kongo, Afrika Kusini,Palestina, Malawi, Marekani, Uganda, nk.