Miaka
ya karibuni wananchi wengi- hususan
vijana- wameulizia mahusiano ya kimapenzi na wageni hasa Wazungu. Hayakuanza leo, jana wala juzi.
Yamekuwapo daima. Ukweli idadi fulani ya watu wa mataifa yote duniani hutaka
kuwa na mahusiano na wageni. Mosi, kutaka kuondokana na udhia wa wananchi wenzao;
pili, kutafuta maisha bora; tatu,mapenzi na ndoa na nne, udadisi (kipya
kinyemi).
Mwandishi nikitumbuiza ngoma wakati wa Carnival la London, Agosti, 2012.
Picha na Urban Pulse Creative Media
Miaka
arobaini au hamsini iliyopita nakumbuka waliopenda mahusiano na wageni walikuwa
zaidi wanaume. Wanawake waliojamiiana na wageni waliitwa malaya, na wachache ni
wale tu waliofanya kazi mahoteli makubwa ya kitalii kutafuta ajira. Mathalan
nakumbuka miaka ya Sitini na Sabini, Tanzania ilijazana wakimbizi. Sera ya TANU
na siasa ya Azimio la Arusha ilisaidia walioathirika na udhalimu wa kikoloni,
ubaguzi nk. Toka Kongo, Afrika Kusini,Palestina, Malawi, Marekani, Uganda, nk.
