Showing posts with label Waafrika na Mapenzi. Show all posts
Showing posts with label Waafrika na Mapenzi. Show all posts

Monday, 18 August 2014

KWA WANAOLILIA MAPENZI NA WAGENI AU WAZUNGU- Sehemu ya 2...


 Karibuni rafiki yangu Mzungu alikuwa Afrika.
Taaluma yake ni uanahabari.  Anaipenda sana Afrika na watu wake. Zamani babu aliishi India na alipinga sana ukoloni. Ana mke  na watoto wawili. Shughuli zake humzungusha kila sehemu.  Analijua bara kuliko hata tuliozaliwa huko.  Baada ya  sifa na vicheko, ghafla alisuta mapenzi.
“Ningekuwa mmoja wa babu zenu zamani Bwana Freddy ningenyaka wake ishirini. Kila  nilikokwenda sikukosa sahiba.  Wanataka niwatumie tikiti za ndege. Waje Ulaya waishi raha mustarehe. Ni vigumu sana kuwahimiza dada hawa kwamba maisha yangu si ya kitajiri. Hata ningekuwa tajiri kwetu Ulaya ndoa za mitala haziruhusiwi.  Na mke wangu hatofurahi akisikia nina wake wengine!”
Inachekesha alivyosema, lakini ndiyo kichuguu cha mchwa hicho.