Showing posts with label Maisha Marefu. Show all posts
Showing posts with label Maisha Marefu. Show all posts
Sunday, 21 April 2013
Monday, 7 February 2011
HAJA NDOGO NJE KWA WANAWAKE SI JAMBO RAHISI...
Tupo sebuleni kwa jirani yangu mmoja mwanamke. Katualika majirani kusherehekea siku ya kuzaliwa miaka themanini. Themanini nakwambia! Wanawe wawili wamewasili na wajukuu na vitukuu toka Australia na Afrika Kusini kushangilia siku hii maalum ya ajuza mcheshi, roho safi; kibibi anayependwa na kila mtu hapa mtaani ninapoishi London. Nyumba imetota baraka. Harufu mbalimbali za makulaji zinazitesa pua. Vyakula vimetandazwa mezani. Viazi Ulaya vya kuchemsha na kuoka vinavyotengeneza msosi maarufu uliovum buliwa na hawa hawa Waingereza unaojulikana kama Chips. Mboga mbichi safi za saladi, nyanya, matango, vitunguu, jibini (chizi), mikate ya kila sampuli, samaki na kuku wa kukaanga. Kawaida karamu za Majuu hutenganisha walaji wa nyama na wasiokula nyama (Vegetarians).
Subscribe to:
Posts (Atom)

