Showing posts with label Maisha Marefu. Show all posts
Showing posts with label Maisha Marefu. Show all posts

Sunday, 21 April 2013

WATU WEUSI TWAKUMBUSHWA MADHARA YA ULAJI CHUMVI NYINGI



Ladha ni kitu muhimu sana.

Siku moja nilikuwa nimealikwa karamu fulani kubwa- mwenyeji ni Mzungu aliyemwoa bibi wa Kiafrika. Kufumba na kufumbua dada mmoja, (sikumbuki taifa lake, lakini alikuwa Mwafrika)-hakuwa na raha hata kidogo na misosi. Kawaida ukialikwa hizi karamu za kimataifa, si mara zote utakuta vyakula vya kwenu; ulivyozoea. Mathalan, Wazungu wanavyokula ni tofauti sana na sisi. Hutumia vitu ambavyo si mazoea yetu mfano jibini (chizi), kachumbari nzito (“mayonnaise”) yenye mayai, siki, mafuta, malai (“cream”), nk. Au kuna suala la nyama.

Siku hizi idadi ya wasiopenda nyama jamii zilizoendelea imekua kubwa kiasi ambacho ukihudhuria mikutano au makongamano ya kimataifa unaulizwa (kabla) je mlaji nyama au hapana.Basi dada hakua na raha.Meza zilijazana vyakula vya wanga, mboga, nyama na protini. Dada alilalamika ladha.


Monday, 7 February 2011

HAJA NDOGO NJE KWA WANAWAKE SI JAMBO RAHISI...

Tupo sebuleni kwa jirani yangu mmoja mwanamke. Katualika majirani kusherehekea siku ya kuzaliwa miaka themanini. Themanini nakwambia! Wanawe wawili wamewasili na wajukuu na vitukuu toka Australia na Afrika Kusini kushangilia siku hii maalum ya ajuza mcheshi, roho safi; kibibi anayependwa na kila mtu hapa mtaani ninapoishi London. Nyumba imetota baraka. Harufu mbalimbali za makulaji zinazitesa pua. Vyakula vimetandazwa mezani. Viazi Ulaya vya kuchemsha na kuoka vinavyotengeneza msosi maarufu uliovum buliwa na hawa hawa Waingereza unaojulikana kama Chips. Mboga mbichi safi za saladi, nyanya, matango, vitunguu, jibini (chizi), mikate ya kila sampuli, samaki na kuku wa kukaanga. Kawaida karamu za Majuu hutenganisha walaji wa nyama na wasiokula nyama (Vegetarians).