
Ladha ni kitu muhimu sana.
Siku moja nilikuwa nimealikwa karamu fulani kubwa- mwenyeji ni Mzungu aliyemwoa
bibi wa Kiafrika. Kufumba na kufumbua dada mmoja, (sikumbuki taifa lake, lakini
alikuwa Mwafrika)-hakuwa na raha hata kidogo na misosi. Kawaida ukialikwa hizi
karamu za kimataifa, si mara zote utakuta vyakula vya kwenu; ulivyozoea.
Mathalan, Wazungu wanavyokula ni tofauti sana na sisi. Hutumia vitu ambavyo si
mazoea yetu mfano jibini (chizi), kachumbari nzito (“mayonnaise”) yenye mayai,
siki, mafuta, malai (“cream”), nk. Au kuna suala la nyama.
Siku hizi idadi ya wasiopenda nyama jamii zilizoendelea imekua kubwa kiasi
ambacho ukihudhuria mikutano au makongamano ya kimataifa unaulizwa (kabla) je mlaji
nyama au hapana.Basi dada hakua na raha.Meza zilijazana vyakula vya wanga, mboga, nyama na protini. Dada alilalamika
ladha.