Showing posts with label Wanawake Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Wanawake Tanzania. Show all posts

Monday, 16 June 2014

USIKU KUCHANGIA JENGO LA WASICHANA WANAOKWEPA UKEKETAJI TANZANIA


Niko hoteli kubwa la The Russet, katikati ya maskani ya wafanyakazi wa kawaida, kaskazini ya  London. Nimealikwa kutumbuiza ngoma za Kiafrika. Mauzo ya sherehe hizo yatasaidia kijiji kimoja Tanzania. Watayarishaji ni shirika la urafiki baina ya Uingereza na Tanzania, BTS yaani British Tanzania Society. Janet Chapman na mwenzake Jonathan Pace, ni wale wazungu wachache wanaofikiria mazuri tu kuhusu Waafrika, hususan Watanzania.
  Watu wa makamo.
Miaka 30 iliyopita  Janet alifanya kazi ya ualimu Sudan,  vijijini; akichanganyika na wakulima na wafugaji maskini. Kati ya jambo ambalo hakulipenda ni mila ya kuwatahiri wasichana wadogo au kwa Kiswahili cha kileo, ukeketaji.  Janet anasema kwa kuwa mwenyewe alikuwa na mabinti wadogo wawili- ambao leo wameshakuwa watu wazima- yalimgusa sana. Baadaye aligundua adha hii imeenea nchi nyingi   bara Afrika, Mashariki ya Kati na Asia.

 Takwimu za shirika la Afya duniani (WHO) zinakadiria wasichana na wanawake milioni 91 na nusu barani wamekeketwa. Kati ya hawa milioni 12 na robo wana umri mdogo wa miaka 10 hadi 14.  Tovuti la habari za ukeketaji (FGM) linadai nchi 26 za Kiafrika, ikiwemo Tanzania zinabeba bendera ya ukeketaji. WHO inafahamisha kati ya wanaotetea adha hii ni mama wazazi waliokeketwa na  baadhi ya wanaume.

Sunday, 31 July 2011

ANNA LUKINDO: MBUNIFU MAVAZI NA MITINDO ANAYEKUZA JINA LA WANAWAKE WA KITANZANIA LONDON

Hebu turudi nyuma miaka 30.
Tanzania ndiyo imemaliza vita kumwondoa Jemadari Idi Amin Dada ; maisha magumu maana serikali imetumia mabilioni ya shilingi kununua silaha kujenga jeshi imara kuwasaidia Waganda. Bidhaa adimu madukani. Hata chakula kinacholimwa nchini (mathalan unga) kazi kukipata. Utata.
 Licha ya kitatange na mahangaiko maelfu ya wakimbizi wamekaribishwa nchini toka  Afrika Kusini, Angola, Namibia na hiyo Uganda yenyewe. Kisiasa Watanzania waungwana sababu ya uongozi wa Mwalimu Nyerere aliyeujua wajibu wake wa kijadi kwa Waafrika wenzetu.  Ni kipindi hiki ndipo miye na wenzangu watatu tulipounda bendi ya mseto wa fasihi na muziki tukaiita “House of Africa.” Ilikuwa vigumu kumpata mwanamke maana enzi hizo jamii yetu iliwabeza kina dada waliofanya sanaa.
Imetolewa pia safu ya "Kalamu toka London" kila Jumapili, gazeti la Mwananchi:
Waliitwa mabahaluu, wavuta bangi, machangu doa; kuimba jukwaani hakukuwa na heshima wala ajira kama walivyo Kizazi Kipya leo...Wakati sisi tukihangaika, Anna Lukindo alikuwa akionyesha mavazi hoteli ya Kilimanjaro, Dar es Salaam siku za wikiendi. Kikazi aliajiriwa na kampuni ya kusanifu nyumba barabara ya Mkwepu. Bado mdogo ana miaka 19, lakini mchapa kazi ile mbaya.
Anna Lukindo akiwa kazini. Anayevalishwa ni mwanamitindo, mpiga picha na mwanabloga, Jestina George . Picha na See Li.

<--more--!> 

Monday, 25 July 2011

BLOG LA “MWANAMKE NA NYUMBA” MFANO WA UANDISHI UNAOANGALIA MAHUSIANO NYETI YA MTANZANIA...

Uandishi wa mablogu wahitaji tarakilishi. Tarakilishi ni neno fasaha la Kiswahili linaloimanisha Kompyuta. Na hiki si chombo tu cha kuandikia. Huendesha simu za mkononi; taa zinazoongoza magari barabarani, mitambo ya ndege, mahospitali, runinga, nk. Dunia ya leo inaongozwa na tarakilishi. Hili ni bado somo jipya Tanzania. Kidunia mtandao kama tunavyoujua una miaka 15 ingawa sayansi hii ya kihabari imekuwepo kwa takribani miaka 30. Awali ilitumiwa na watu wachache hasa wanajeshi na majasusi kulinda matakwa ya serikali mbalimbali.
Rosemary Mizizi, blog lake Mwanamke na Nyumba linazungumzia mahusiano nyeti kati ya wanawake na wanaume  kwa undani sana katika jamii ya Tanzania leo.
<--more--!>