Showing posts with label Historia na Dini. Show all posts
Showing posts with label Historia na Dini. Show all posts

Sunday, 22 June 2014

KISWAHILI NA MAHUSIANO YETU NA UTAMADUNI WA KIARABU


 Shangwe zilizoenea Ulaya nzima sasa hivi ni mashindano ya soka, Brazil.
 Ila wasiwasi uliowashika wanausalama wanaojua mikunjo kunjo ya shuka na kanzu za ulimwengu wetu ni tafrani kali zinazoendelea Syria na Iraq. Wasiwasi wa  mashushushu na wanasiasa Majuu ni hatari zitakazoenezwa na migogoro hii. 
 Uingereza mathalan imedai  vijana 400 wazawa  hapa, wanapigana Syria. Wakimaliza watarejea na kusambaza ugaidi  ulimwenguni.  Vyombo kadhaa vya habari Uingereza vimeonya jinsi mamia ya vijana wake wanavyomenyana pia Iraq,  Libya, Afghanmistani, Kenya na Somali  alipo mwanamke wa Kizungu anayetafutwa kuliko fedha.
Samantha, mmoja wa wanae na mumewe gaidi aliyehusika na mauaji ya London 2005. Picha toka gazeti la Mirror

 Samantha Lewthwaite, alikuwa mke wa mmoja wa magaidi wanne waliolipua mabomu na kuua  watu 51 mjini London mwaka 2005. Inadaiwa Septemba 2013, magaidi wa Al Shabaab (walipoua  67 na kujeruhi 175),  Nairobi, Mwingereza huyu mwenye watoto wanne alihusika.  Inadaiwa keshasilimu (anaitwa Sherafiya) na kuolewa na mmoja wa viongozi wakubwa wa Al Shabaab, Hassan Maalim Ibrahim.  Al Shaabab maanake ni “vijana” kwa Kiarabu, ilhali  Boko Haram  ni Elimu ya Kizungu ni Haram.
 Mauaji ya makundi haya  hufanywa  kwa madai eti yanatukuza Uislamu.

Thursday, 13 December 2012

NINI MIZIZI YA TATIZO LA WAISLAMU KUCHOMA MAKANISA NA AMANI AFRIKA?-Sehemu ya 2


 Jumapili iliyopita tuliona namna mwanamuziki Fela Kuti  alivyoonya kuhusu imani za kigeni zilivyochangia kupotosha utamaduni wa Mwafrika.
Akasisitiza : “Ukristo na Uislamu si dini zetu...Wakristo wana fikra na tabia  za Waingereza na Wamarekani, ilhali Waislamu wana tabia za Waarabu.” 
 Msikilize mwenyewe akijieleza kinaga naga
Jadi mbalimbali duniani  zilijengwa kufuatana na mazingira na hali ya hewa. Dini zilitumia mvua, jua, radi, miti, wanyama nk,  kuabudu na kutambika.  Dini mbili kuu za Waafrika leo zimetokana na utamaduni wa Mashariki ya Kati na Wazungu.


<--more--!>