Showing posts with label Dini na Siasa. Show all posts
Showing posts with label Dini na Siasa. Show all posts

Thursday, 13 December 2012

NINI MIZIZI YA TATIZO LA WAISLAMU KUCHOMA MAKANISA NA AMANI AFRIKA?-Sehemu ya 2


 Jumapili iliyopita tuliona namna mwanamuziki Fela Kuti  alivyoonya kuhusu imani za kigeni zilivyochangia kupotosha utamaduni wa Mwafrika.
Akasisitiza : “Ukristo na Uislamu si dini zetu...Wakristo wana fikra na tabia  za Waingereza na Wamarekani, ilhali Waislamu wana tabia za Waarabu.” 
 Msikilize mwenyewe akijieleza kinaga naga
Jadi mbalimbali duniani  zilijengwa kufuatana na mazingira na hali ya hewa. Dini zilitumia mvua, jua, radi, miti, wanyama nk,  kuabudu na kutambika.  Dini mbili kuu za Waafrika leo zimetokana na utamaduni wa Mashariki ya Kati na Wazungu.


<--more--!>