Kwanza kabla ya kuendelea na (kumalizia) mada tuliyoianza
wiki jana, tuwape pole ndugu wa familia
yake Albert Mangwea. Tuwape pia pole marafiki zake na wote waliomjua kwa
karibu. Tuwaombe radhi kwa kuendelea kuzungumzia jambo ambalo linawakumbusha
uchungu wa mtu aliyekwisha zikwa.
Pamoja na hayo tujikumbushe madhumuni ya kuandika na
kuzungumzia suala hili.
Kwanza kabisa kupoteza vijana wanaoanza maisha katika
hali hizi mbaya si jambo zuri. Wapo wengi wanaondelea kuzungumzia kwamba ni
Mungu kaamua na kwamba kifo ni asili maisha. Hatukatai hilo. Ila kwetu Tanzania
imekua sasa desturi kukubali vifo na utamaduni wa kufa mapema. Wanapoendelea kufariki vijana tunakubali ni
maajaliwa. Zikitokea ajali za magari (zinazouzilika) zilizotokana na
uzembe wa madereva pia tunalitaja jina
la Mungu. Mungu amekuwa sasa ndiye mwamba wa kila baya. Kageuka kisingizio.
Kwanini sisi tu ndiyo kitakwimu tuna vifo vingi zaidi tena vya watu wenye umri
mdogo?
Lakini kabla ya kuendelea zaidi, tukubaliane ...