Showing posts with label Fasihi na Ulevi. Show all posts
Showing posts with label Fasihi na Ulevi. Show all posts

Monday, 17 June 2013

KIFO CHA ALBERT MWANGEA -KINATUULIZA MASWALI GANI?- Sehemu 1



Babu wa fasihi ya Kiswahili, Shaaban Robert alifariki mwezi huu  mwaka 1962. Ingetakiwa sikukuu ya kifo  chake yaani Juni 20  ifanyiwe maadhimisho kila mwaka. Sisi na wenzangu wa bendi ya Sayari tuliwahi kusheherekea kwa maonyesho ya 1983. Hazina hii tukufu ya taifa inatakiwa zaidi ya hilo.
  Moja ya vitabu vyake babu ni  “Kielezo cha Fasili” (kilitolewa upya na mwongozi wa wachapishaji Tanzania; “Mkuki na Nyota” ,2004) kinafafanua mashairi yake kwa wasomaji mintaarafu  ya kujenga mapafu kilugha.
Ananyambua  Shairi la “Jina”: “Mwanadamu mwenye fikra njema huacha fahari au sifa kwa watu ambayo vizazi vyake vya nyuma yake hupenda kuiona, na ambayo itakuwa kama hazina kwa watu wote katika dunia.”
Albert Mangwea hakua Shaaban Robert;  kafa akiwa na miaka 31 tu. Lakini  Mangwea au Mangair alitumia fani ya ushairi kuchangia kuiendeleza fasihi ya Kiswahili  na kipaji chake alichomegewa na Muumba.
Kifo  hiki kilichokua Usauzi (Afrika Kusini) kimeongelewa na kinaendelea kuongelewa. Mwaka jana wakati huu Tanzania ilimpoteza Steve Kanumba. Vifo vya chipukizi hawa vimeacha utata na mijadala marefu.
 Mangwea alifia ughaibuni.  Maisha ugenini ni magumu maana habari huwa hazitangazwi sana. Mbali na taratibu za kisheria na itikeli, kinachongojewa kutufariji huwa viongozi wa dini na serikali.