Showing posts with label Afrika na Afya. Show all posts
Showing posts with label Afrika na Afya. Show all posts

Wednesday, 12 October 2016

VIPI TATIZO LA FIGO LAZIDI KUATHIRI AFYA ZA WAAFRIKA? - Sehemu 1



Tiba na afya za dunia yetu zimegawanyika sehemu mbili kuu.
 Magharibi ni uganga wa Kizungu unaotumia sayansi iliyofikia kilele karne ya 19 na 20. Moja ya nguzo zake kuu ni kutibu kwa kunyamazisha- kupitia sindano, dawa na upasuaji. Tiba ya Kizungu ndiyo inayotawala dunia yetu na ndiyo mara nyingi Wabongo wanaojiweza wakiugua siku hizi husafrishwa nje  kutibiwa.
Tiba za mashariki zinaongozwa na ustaarabu wa Kihindi na Kichina. Wahindi hutumia mwenendo uitwao Ayurveda. Tiba hii yenye zaidi ya miaka elfu mbili huangalia mwili mzima ukoje kabla ya kuushughulikia. Wachina wanao pia mtindo huo huo, unaotazama mtiririko wa nguvu mwilini badala ya dosari. Utaratibu wa Kichina na Kihindi kijumla hautibu tatizo moja kama  Wakizungu. Kwa wazungu mathalani ukiumwa kichwa utapewa dawa ya kuyaondoa maumivu hayo.

Sunday, 30 November 2014

TEZI KIBOFU, AFYA NA KINGA YA MARADHI YANAYOTUKABILI -sehemu ya 1




Wiki hii,  Mheshimiwa Rais J Kikwete, alikuwa Marekani kufanyiwa matibabu ya tezi ya uume, hospitali ya John Hopkins,  Baltimore. Kitakwimu maradhi haya huwafika asilimia 45 ya wanaume walioshapitisha miaka 60.   Ingawa lengo la makala haya si kuzungumzia hali ya Rais, ni vizuri tukitathimini tatizo hili linalowasakama wanaume wengi. Miongoni mwa walioshafikwa ni marehem Nelson Mandela, kiongozi wa Waislamu Marekani, Louis Farahkan, mwanamuziki maarufu hayati James Brown, mwigizaji mashuhuri wa Hollywood, Robert De Niro, nk.
Miaka michache iliyopita niliwahi kuandika juu ya afya ya uume ( na uke vile vile) na kuhimiza haja ya kuelewa namna ya kutunza na kufanya mazoezi kutunza viungo hivi. Kwa wanaume viungo viwili muhimu husika ni mfuko wa mbegu (korodani) na tezi kibofu. Visipoangaliwa vyema husababisha saratani ambayo kihisabati,  inaua mwanaume mmoja kati ya  saba, duniani. Moja ya suluhisho kuu ni kuzifahamu dalili   kabla hazijaota kutu.  
Lakini tezi ya uume au tezi kibofu, ni nini hasa?