Tiba na afya za dunia yetu zimegawanyika sehemu mbili
kuu.
Magharibi ni
uganga wa Kizungu unaotumia sayansi iliyofikia kilele karne ya 19 na 20. Moja
ya nguzo zake kuu ni kutibu kwa kunyamazisha- kupitia sindano, dawa na
upasuaji. Tiba ya Kizungu ndiyo inayotawala dunia yetu na ndiyo mara nyingi
Wabongo wanaojiweza wakiugua siku hizi husafrishwa nje kutibiwa.
Tiba za mashariki zinaongozwa na ustaarabu wa Kihindi na
Kichina. Wahindi hutumia mwenendo uitwao Ayurveda. Tiba hii yenye zaidi ya
miaka elfu mbili huangalia mwili mzima ukoje kabla ya kuushughulikia. Wachina
wanao pia mtindo huo huo, unaotazama mtiririko wa nguvu mwilini badala ya
dosari. Utaratibu wa Kichina na Kihindi kijumla hautibu tatizo moja kama Wakizungu. Kwa wazungu mathalani ukiumwa kichwa
utapewa dawa ya kuyaondoa maumivu hayo.
