Showing posts with label Magonjwa Muhimu. Show all posts
Showing posts with label Magonjwa Muhimu. Show all posts

Wednesday, 12 October 2016

VIPI TATIZO LA FIGO LAZIDI KUATHIRI AFYA ZA WAAFRIKA? - Sehemu 1



Tiba na afya za dunia yetu zimegawanyika sehemu mbili kuu.
 Magharibi ni uganga wa Kizungu unaotumia sayansi iliyofikia kilele karne ya 19 na 20. Moja ya nguzo zake kuu ni kutibu kwa kunyamazisha- kupitia sindano, dawa na upasuaji. Tiba ya Kizungu ndiyo inayotawala dunia yetu na ndiyo mara nyingi Wabongo wanaojiweza wakiugua siku hizi husafrishwa nje  kutibiwa.
Tiba za mashariki zinaongozwa na ustaarabu wa Kihindi na Kichina. Wahindi hutumia mwenendo uitwao Ayurveda. Tiba hii yenye zaidi ya miaka elfu mbili huangalia mwili mzima ukoje kabla ya kuushughulikia. Wachina wanao pia mtindo huo huo, unaotazama mtiririko wa nguvu mwilini badala ya dosari. Utaratibu wa Kichina na Kihindi kijumla hautibu tatizo moja kama  Wakizungu. Kwa wazungu mathalani ukiumwa kichwa utapewa dawa ya kuyaondoa maumivu hayo.