Mara ya kwanza kuvaa mkanda katika gari ilikuwa nilipopewa lifti na Mzungu mmoja miaka ya Sabini. Kipindi hicho tuliwaita weupe, walami. Sijui neno lilitokea wapi. Ila yupo jamaa aliyefasiri kuwa “mlami” ilitokana na “lami” yaani barabara safi, isiyo ya matope, makorongo, udongo au mchanga. Barabara iliyowekwa lami ikawa ya Kizungu zungu. Na enzi hizo, walami waliangaliwa kama watu walioendelea. Si tu kitabia pia kiteknolojia. Ukiwa na mlami, unaulizwa maswali. Kakupa nini? Kakupeleka wapi, mlami? Atakupeleka mtoni? Yaani, utofauti.

