Vitendo viwili
vichafu “vinavyofichwa” na watawala
duniani ni biashara ya dawa za kulevya na unyanyasaji wa watoto. Ingawa vya aibu na ufidhuli vina faida sana kwa
wahusika. Dawa za kulevya ni biashara inayotajirisha haraka kuliko zote.
Ripoti
iliyotolewa na Idara ya Kuzuia Uhalifu na Dawa za Kulevya ya Umoja wa Mataifa
(UNIDOP) mwaka 2011, inasisitiza asilimia
20 ya kipato cha dunia hutokana na
biashara hii ya ki-Ibilis. Ndiyo maana mtu yeyote anapopambana na ujambazi huu
lazima atauawa. Haya yanaonekana Mexico - kilele cha ujambazi wa dawa za
kulevya. Video za mauaji – wakiwepo wanawake na vigoli- wakikatwa katwa kwa mapanga, visu na mashoka zimeselelea
mitandaoni.
Habari za Watanzania waliokamatwa wakibeba
unga au “heroin” ughaibuni sasa zimekuwa nongwa.
Unyanyasaji wa
watoto hauna faida ya kiuchumi ila ni “jaha” kwa wahusika. Hali kadhalika ni rahisi kuwatumia watoto kubeba silaha, mizigo, kuwalawiti nk.