Showing posts with label Unyanyasaji wa kifamilia. Show all posts
Showing posts with label Unyanyasaji wa kifamilia. Show all posts

Sunday, 30 November 2014

VITA DHIDI YA KULAWITI NA KUBAKA WATOTO VYAWAKA MOTO UZUNGUNI – Sehemu ya 2





Vitendo viwili vichafu  “vinavyofichwa” na watawala duniani ni biashara ya dawa za kulevya na unyanyasaji wa watoto. Ingawa  vya aibu na ufidhuli vina faida sana kwa wahusika. Dawa za kulevya ni biashara inayotajirisha haraka kuliko zote.
Ripoti iliyotolewa na Idara ya Kuzuia Uhalifu na Dawa za Kulevya ya Umoja wa Mataifa (UNIDOP) mwaka 2011, inasisitiza  asilimia 20 ya  kipato cha dunia hutokana na biashara hii ya ki-Ibilis. Ndiyo maana mtu yeyote anapopambana na ujambazi huu lazima atauawa. Haya yanaonekana Mexico - kilele cha ujambazi wa dawa za kulevya. Video za mauaji – wakiwepo wanawake na vigoli- wakikatwa katwa  kwa mapanga, visu na mashoka zimeselelea mitandaoni.
 Habari za Watanzania waliokamatwa wakibeba unga au “heroin” ughaibuni sasa zimekuwa nongwa.
Unyanyasaji wa watoto hauna faida ya kiuchumi ila ni “jaha” kwa wahusika.  Hali kadhalika ni rahisi kuwatumia watoto  kubeba silaha, mizigo, kuwalawiti nk. 

VITA DHIDI YA KULAWITI NA KUBAKA WATOTO VYAWAKA MOTO UZUNGUNI




 Leo tuzungumzie watoto. Tuangalie afya, mapenzi na usalama wao. Hakuna kipindi cha historia yetu wanadamu ambapo watoto wanafanyiwa  unyama duniani kama sasa.
Mwezi Machi,  Shirika la Umoja wa Mataifa la Hazina ya Watoto (UNICEF) lilisema tangu vita vianze Syria,  watoto 10,000, wameuawa  makusudi. Wengine milioni tano hawana makazi maalum.  Mauaji haya yanafanywa  majumbani,  mashuleni, mitaani na  kambi za wakimbizi. Watoto wanapigwa risasi makusudi na magaidi wa Boko Haram, Nigeria. Miezi miwili sasa wasichana  200 waliotekwa mkuku na wanaharam hawa (wanaotumia dini kama ngao ya uyahawani wao) hawajapatikana. Kila kukicha watoto vijijini na mashuleni Nigeria wanauliwa bila hatia yeyote.