Sijui wasomaji wangapi tunamkumbuka
mwanamuziki mashuhuri wa Nigeria, Fela Anikulapo Kuti aliyefariki 1997 akiwa na
umri wa miaka 59? Fela alikuwa binam wa
mwandishi maarufu, Wole Soyinka (pichani) aliyeshinda tuzo la fasihi (Nobel) duniani 1986.
Pamoja na kipaji cha muziki
(utunzi wenye ujumbe mzito, kuimba, kupiga saxafoni, ngoma na piano) Fela hakua
mwoga. Alikuwa mmoja wa wanamuziki
wachache Afrika ambaye hakusita si tu kuimba ukweli, bali tayari kupambana na
serikali ya nchi yake na kukemea ufisadi na rushwa vilivyoinyea(na bado
vinaendelea) Nigeria.
Serikali na majeshi
yalimchukia na kumwandama kiasi ambacho mwaka 1977 askari elfu moja walivamia
makao makuu ya bendi yake -Afrika 70-
wakampiga yeye, wake zake na wanabendi halafu wakaharibu kila kitu. Ndani ya vurugu hiyo
walimtupa mamake Fela (Funmilayo) dirishani – baadaye akafia hospitalini. Fela
aliudhika sana akatunga nyimbo mbili
kuishutumu serikali na askari wadhalimu (“Coffin for Head of State” na “Unknown
Soldier”) na kulipeleka jeneza la mama mzazi makao makuu ya jeshi yaliyoongozwa
na Jenerali Olusegun Obasanjo(aliyekuja kuwa Rais). Licha ya kipigo, baadaye alitafutiwa vijisababu akafungwa jela
miaka mitano kwa msimamo usiokua na woga wala unafiki.
Tuangalie dhana ya unafiki.
Fela Kuti alioa wake 27 (aliowaita
malkia ), mwaka 1977; waliimba na
kucheza naye jukwaani.
<--more--!>
<--more--!>