Enzi hizo hatukua na UKIMWI.
Magonjwa ya zinaa hayakuua mtu. Dalili yake ilikuwa
kuwashwa na kujisikia vibaya wakati wa kwenda haja ndogo tu, basi. Yakikuzidia
unazunguka zunguka mitaani unanunua dawa rangi ya chungwa na manjano- kidonge cha
“tetracylene”- aghali ndiyo; lakini kinamaliza kabisa tatizo.
Baadaye miaka ya Themanini UKIMWI ukatangaza ufalme.
UKIMWI haukuponywa kwa kidonge kama hicho.
Na hata baada ya
miaka thelathini, UKIMWI uliposhaanza kutibika- ( nchi zilizoendelea), haikua
kidonge kimoja. Vingi. Tena bei yake si
ya porojo. Sijasikia mtu anayeweza kuingia tu sehemu akanunua msururu wa
vidonge vya kutibu UKIMWI. Tiba hii ilihimili lakini haijaondoa kirusi, abadan.
