Showing posts with label Kiarabu na Kiswahili. Show all posts
Showing posts with label Kiarabu na Kiswahili. Show all posts

Sunday, 24 March 2013

USONGO WANGU NA KISWANGLISHI : WATANZANIA HATUJAKOMAA KILUGHA- 1


Karibuni, Baraza la Waganga Uingereza lilipitisha sera ya kutomruhusu daktari wa kigeni kufanya kazi bila kufuzu mtihani wa Kiingereza fasaha. Ina maana ili kutibu wagonjwa lazima uimanye lugha ya wenyeji vizuri. Wenyeji wanathamini sana lugha yao mama- bila kuichanganya nganya na kuibandika  bandika viraka.
Mwandishi maarufu wa Kiswahili fasaha, Adam Shafi akiwa Uingereza mwaka 2007. 
Picha na F. Macha

Msemaji wa Baraza hilo alipohojiwa na runinga ya “Sky” alijitoa mwenyewe kama mfano:
“Nilisoma Kifaransa nikiwa sekondari. Ninaweza kuongea Kifaransa cha kuombea maji. Ila nilipofanya kazi kwao  kama mganga nlikua na matatizo maana sikuyajua maneno au misemo ya taaluma ya uganga ipasavyo. Ikabidi niende kozi. Ni hatari sana kutibu watu kama unaboronga lugha.”
Akiwa na maana kujua lugha juu juu au sawasawa ni mambo mawili tofauti. Wenzetu waliondelea wanathamini sana kufahamu lugha sawasawa badala ya kubabaisha.
Nimetathmini sera hiyo ya Waingereza ili kuongelea suala la Ki-Swanglish ambacho kinaendelea kuzaa chawa Tanzania. Miezi michache iliyopita nilikua kwenye kikao na kundi la Wabongo wenzangu hapa Ulaya, mzalendo mmoja akauliza: “ Bwana Macha hapendi sana kuchanganya changanya maneno ya Kiingereza na Kiswahili.”
Kitabu kipya cha Adam Shafi- kinachoendeleza Kiswahili Fasaha. Picha toka Blog la KiSwahili Afrika Mashariki