Showing posts with label Dawa za Kulevya na Maendeleo. Show all posts
Showing posts with label Dawa za Kulevya na Maendeleo. Show all posts

Sunday, 30 November 2014

MJADALA WA MADHARA YA UVUTAJI BANGI WAPAMBA MOTO UINGEREZA




Bangi.
Neno lenye maana na majina mengi. Marijuana. Cannabis. Sigara kali.  Spliff. Kaya. Na kadhalika. Kwa Kiswahili asili ya neno “bhang” ni Kihindi. Sina hakika kama zamani kabla ya ujio wa wageni tulilienzi jani hili. Jani lililo mkebe mmoja na “kunguni” wa dawa za kulevya. Heroin. Unga wa Cocaine. Na mengineyo.  Dawa zinazomgeuza mwanadamu dude, afriti,  mahoka,  jambazi. Dawa zenye uwezo wa kuharibu  jamii  kama ilivyo Mexico sasa hivi. Unabisha? Ingia, You Tube.
Uuone uhayawani wa dawa za kulevya ulivyoshawabadili wanadamu   mafisi. Kuwapeleka wake, mabinti na dada za majambazi wenzao mwituni kuwafyeka shingo na mashoka. Tunaambiwa magaidi wa ISIS huko Syria na Iraq, hukata shingo. Mexico hukatakata mwili vipande vipande  kisha wakaviacha viozee vichakani mithili ya vinyesi.
Hebu tafakari  ufisi kama huu ujipenyeze Tanzania. Ndiyo mwisho. Hatuna tena nchi ya amani wala kuingia mitaani wikiendi kula nyama choma; kuzamia misikitini, jamatini au makanisani. Ni harufu ya damu kila mahali. Ulaghai kwisha kazi. Hamnazo.
Sasa bangi...