Bangi.
Neno lenye maana na majina
mengi. Marijuana. Cannabis. Sigara kali. Spliff. Kaya. Na kadhalika. Kwa Kiswahili
asili ya neno “bhang” ni Kihindi. Sina hakika kama zamani kabla ya ujio wa
wageni tulilienzi jani hili. Jani lililo mkebe mmoja na “kunguni” wa dawa za
kulevya. Heroin. Unga wa Cocaine. Na mengineyo.
Dawa zinazomgeuza mwanadamu dude, afriti, mahoka, jambazi. Dawa zenye uwezo wa kuharibu jamii kama ilivyo Mexico sasa hivi. Unabisha? Ingia,
You Tube.
Uuone uhayawani wa dawa za
kulevya ulivyoshawabadili wanadamu mafisi. Kuwapeleka wake, mabinti na dada za
majambazi wenzao mwituni kuwafyeka shingo na mashoka. Tunaambiwa magaidi wa
ISIS huko Syria na Iraq, hukata shingo. Mexico hukatakata mwili vipande vipande
kisha wakaviacha viozee vichakani
mithili ya vinyesi.
Hebu tafakari ufisi kama huu ujipenyeze Tanzania. Ndiyo
mwisho. Hatuna tena nchi ya amani wala kuingia mitaani wikiendi kula nyama
choma; kuzamia misikitini, jamatini au makanisani. Ni harufu ya damu kila
mahali. Ulaghai kwisha kazi. Hamnazo.
Sasa bangi...